Fidan anasema kuwa mpango wa Israeli wa kufanya machafuko unazidi kuendelea. /Picha: AA  

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan amesisitiza umuhimu wa kuongeza jitihada za kushawishi nchi mbalimbali ziitambue dola ya Palestina.

Kulingana na Fidan, kuahirisha kuitambua Palestina sio suluhu bali kunaiongezea muda Israeli wa kufanya mashambulizi zaidi.

Fidan alitoa ujumbe huo katika Mkutano wa Washirika wa Kimataifa na mkutano wa utekelezaji wa suluhisho la serikali mbili, likiwemo suala la kuitambua Palestina lililofanyika mjini Brussels ndani ya mfumo wa majadiliano yake kuhusu suala la Palestina.

Waziri Mkuu wa Palestina Mohammed Mustafa aliwasilisha vipaumbele na mipango ya serikali yake, akiangazia matarajio yao kwa washirika wa kimataifa, wakati wa mkutano huo.

Mkutano wa pili uliangazia jitihada za kisiasa za suala la Israeli na Palestina na juhudi za kuanzisha dola ya Palestina.

Fidan alifahamisha kuwa kufungia Israeli kupata mapato kutoka kwa Wapalestina ni njia mojawapo ya kuishinikiza Mamlaka ya Ndani ya Palestina, akisisitiza haja ya ufadhili endelevu kwa baraza hilo linaloongoza.

Amesisitiza azma ya Israeli chini ya Benjamin Netanyahu ya kukamilisha mipango ya kuwatokomeza Wapalestina.

Fidan pia amesema kuwa mpango wa utokomezaji wa Israeli unaendelea kutoka Gaza hadi West Bank na Mashariki ya Jerusalem.

Alitambua juhudi zote zilizofanywa kwa ajili ya Palestina tangu Makubaliano ya Oslo lakini akasisitiza kuwa bila kusisitiza juu ya mtazamo tofauti, hakuna matokeo tofauti yanayoweza kutarajiwa.

Palestine sio 'serikali' bali 'mamlaka'

Fidan amesema kuwa jumuiya ya kimataifa inaitambua Palestina kama "mamlaka" na sio "serikali" toka makubaliano ya Oslo, ishara ya kukosekana kwa usawa.

Pia alisisitiza umuhimu wa kuifanya Palestina iwe kama dola kamili yenye taasisi zake zenyewe.

Vilevile aligusia umuhimu wa kuongeza juhudi za kuzifanya nchi zaidi kuitambua dola ya Palestina na kusema kuwa Israeli wasitegemewe kufanya mazungumzo na Wapalestina ili kutambuliwa.

TRT Afrika