| swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Rais wa Sudan Kusini akubali kuongea na upinzani kabla ya uchaguzi
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amekubali kufanya mazungumzo na upinzani kabla ya uchaguzi wa Desemba 2024.
Rais wa Sudan Kusini akubali kuongea na upinzani kabla ya uchaguzi
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir ameweka Disemba 2024 kuwa tarehe ya uchaguzi mkuu wa kwanza nchini humo. / Picha: AA
28 Machi 2024

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemuomba Rais wa Kenya William Ruto kutuma mpatanishi ambaye atashiriki katika kile anachokiita Mchakato wa Usuluhisho wa Amani huko Sudan Kusini.

Kupitia taarifa kutoka kwa Msemaji wa Ikulu ya Kenya Hussein Mohamed, Kiir aliomba mazungumzo hayo yafanyike ili pande zote za serikali tawala na upinzani ziweze kutatua masuala yenye utata kabla ya uchaguzi wa Desemba.

Hii imetokea baada ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar kuomba duru mpya ya mazungumzo kabla ya uchaguzi kufanyika, akisema maendeleo madogo yamefanyika kuhakikisha uchaguzi wa Desemba unakuwa wazi.

"Mazungumzo yanalenga kufikia makubaliano na amani kuelekea uendeshaji wa uchaguzi (wa Desemba)," Mohamed alisema katika taarifa siku ya Alhamisi.

Nyongeza ya Muda

Machar alipendekeza muda wa serikali ya mpito uongezwe ili kuruhusu maandalizi ya kutosha kwa ajili ya uchaguzi, lakini upande wa Kiir umekataa wito wa upanuzi.

Kenya imewateua Kamanda wa Jeshi la Zamani Lazarus Sumbeiywo na Balozi Mohammed Ali Guyo kuongoza mazungumzo hayo.

Pata habari zaidi kupitia whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan