| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Jeshi la Nigeria laua zaidi ya 'magaidi' 100
Vikosi vya usalama vya Nigeria hivi karibuni vimeongeza operesheni dhidi ya makundi yenye silaha nchini humo.
Jeshi la Nigeria laua zaidi ya 'magaidi' 100
Magaidi wa Boko Haram mara nyingi hufanya mashambulizi kaskazini mashariki mwa Nigeria na katika nchi jirani. Picha: Picha za Getty / Others
19 Oktoba 2024

Jeshi la Nigeria liliwauwa magaidi 101 katika wiki iliyopita katika operesheni zilizowalenga Boko Haram, ISWAP na magenge ya uhalifu, afisa mmoja alisema Ijumaa.

Mkurugenzi wa Operesheni za Vyombo vya Habari vya Ulinzi, Meja Jenerali Edward Buba, alithibitisha kuwa jeshi lilifanya operesheni katika mikoa mbalimbali nchini katika wiki iliyopita.

Buba alisema kamanda mmoja wa Boko Haram aliuawa katika operesheni hizo.

Zaidi ya hayo, watu 157 waliokuwa mateka waliokolewa na ''magaidi 182'' walikamatwa.

Wanajeshi walikamata silaha 71, magari mawili na kiasi kikubwa cha risasi.

Nigeria imekuwa ikipambana kwa muda mrefu na mashambulizi kutoka kwa makundi yenye silaha, ikiwa ni pamoja na Boko Haram na ISWAP, hasa katika maeneo ya kaskazini mwa nchi.

Licha ya hukumu ya kifo kwa utekaji nyara, utekaji nyara kwa ajili ya fidia bado ni jambo la kawaida kote nchini.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika