MICHEZO
1 dk kusoma
Namibia na Zimbabwe zafuzu kwa Kombe la Dunia la Kriketi T20 mwaka 2026
Zimbabwe imeungana na Namibia katika kufuzu Kombe la Dunia T20 kwa wanaume baada ya kuifunga Kenya kwenye nusu fainali ya pili kwa Afrika mjini Harare. Nchi ya tatu kufuzu ni Afrika Kusini, ambao walipata tiketi ya moja kwa moja kwa Kombe la Dunia.
Namibia na Zimbabwe zafuzu kwa Kombe la Dunia la Kriketi T20 mwaka 2026
Timu ya Kriketi ya Namibia. / Reuters
3 Oktoba 2025

Namibia na Zimbabwe wamejihakikishia nafasi zao kwenye Kombe la Dunia la Kriketi T20 mwaka 2026 baada kutinga fainali za kanda ya Afrika mjini Harare siku ya Alhamisi.

Timu zote mbili zimefuzu kwa mashindano ambayo yatakuwa na wenyeji wenza India na Sri Lanka kati ya mwezi Februari na Machi mwakani.

Namibia iliifunga Tanzania kwa mikimbio 63 katika nusu fainali iliyokuwa na msisimko mkubwa. Zimbabwe nayo ikaigaragaza Kenya katika uwanja wa nyumbani Harare na kuwa timu ya 17 kufuzu kwa Kombe la Dunia T20 mwaka 2026.

Namibia na Zimbabwe watapambana kwenye fainali ya Kanda ya Afrika Oktoba 4, lakini timu zote mbili zimefuzu kwa mashindano ya Kombe la Dunia.

CHANZO:TRT Afrika Swahili