Ijue tofauti ya michuano ya CHAN na ile ya AFCON
AFRIKA
2 dk kusoma
Ijue tofauti ya michuano ya CHAN na ile ya AFCONMichuano ya CHAN 2024, inaandaliwa kwa pamoja na Tanzania, Kenya na Uganda.
Clement Mzize aliifungia Tanzania mabao mawili katika ushindi wao wa 2-1 dhidi ya Madagascar./Picha:Wengine
11 Agosti 2025

Michuano ya CHAN 2024 inaendelea kurindima katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda.

Hadi kufikia sasa, zipo timu zilizofurahia matokeo yao kwenye hatua za makundi, na zipo zile ambazo bado hazijafahamu hatma yao, ndani ya mashindano hayo maalumu kwa wachezaji wanaoshiriki ligi za ndani barani Afrika.

Je, unafahamu tofauti ya michuano ya CHAN na ile Kombe la Mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON?

Ipo hivi.

Wakati michuano ya CHAN ikihusisha wachezaji wanaoshiriki ligi za ndani, michuano ya AFCON hukutanisha wachezaji wa ligi za ndani na nje ya nchi wanazochezea.

 Ngoja nikupe mfano huu.

Kiungo wa Kenya Mohammed Bajaber, alikuwa ni sehemu ya Harambee Stars ambacho kinashiriki CHAN 2024 akiwa na timu ya Kenya Police.

Hata hivyo, ameshindwa kushiriki kwenye michuano ya CHAN, baada ya kusajiliwa na Simba Sports Club ya Tanzania.

Vivyo hivyo kwa Mbwana Samatta na Simon Msuva, ambao wanachezea nje ya Tanzania.

 Ila wachezaji wanaoshiriki ligi za ndani na wale wanaoshiriki ligi za nje, hukutana pamoja kwenye timu zao za taifa, wakati wa michuano ya AFCON.

Wakati michuano ya CHAN ikiwa imeanza mwaka 2009, mashindano ya AFCON yalianza mwaka 1957.

 Vile vile, michuano ya AFCON inatambulika kama mashindano makubwa na yenye hadhi ya kipekee barani Afrika, wakati michuano ya CHAN yanachukuliwa kama jukwaa la kukuza vipaji vya ndani tu.

 Wakati mashindano ya AFCON yakipata msukumo na mguso wa kimataifa, mashindano ya CHAN yamejizoelea umaarufu tu ndani ya bara la Afrika.

Unakumbuka kauli za kocha Jose Mourinho na beki wa zamani wa Liverpool Jamie Carragher?

“Umuhimu wa michuano ya AFCON unazidi kuonekana siku hadi siku. Binafsi, napenda zaidi kuangalia michuano ya AFCON kutokana na uwezo wake wa kuzalisha wachezaji wenye vipaji,” aliwahi kunukuliwa akisema kocha huyo wa klabu ya Fenerbahce inayoshiriki Ligi Kuu ya nchini Uturuki.

 Hali ilikuwa tofauti kwa Carragher, ambaye alikosolewa vikali na wapenda soka barani Afrika, kwa kitendo cha ‘kudogosha’ na ‘kuidharau’ michuano ya AFCON.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32