3 Desemba 2025
Ukipita karibu na ofisi yake ya kushonea, huenda usigundue kuwa mwendeshaji wa ofisi hiyo ana changamoto ya kuona.
“Nimefanya kazi hii kwa miaka 34 sasa, na ndiyo kazi pekee ninayoijua kwa kweli,” anasema Charles Kibe Mwangi, fundi cherehani mwenye changamoto ya kuona, katika mahojiano yake na TRT Afrika.
Huku ulimwengu ukigeuka giza mbele ya macho yake, Charles aligeukia fimbo yake ya ufagio, kama rafiki yake na tegemeo lake pekee anapojaribu kutembea kutoka sehemu moja hadi nyingine.
Hata hivyo, hakuruhusu ulemavu wake kuwa kizuizi kwake katika shughuli za kumpatia riziki yake ya kila siku, yaani ushonaji.

