Kiwango cha biashara kati ya Uturuki na Afrika imefika dola 40.7 za Marekani mwaka 2022 / Picha: AA

Ofisi ya Uwekezaji ya Uturuki imetunukiwa tuzo katika Kongamano la AIM 2024 (Mkutano wa Kila Mwaka wa Uwekezaji) huko Abu Dhabi kwa kuwa mojawapo ya mashirika yenye ufanisi zaidi ya uwekezaji duniani kote kupitia miradi yake endelevu na yenye ubunifu.

Mashirika ya kimataifa ya uwekezaji yalitathminiwa katika kategoria nane: uvumbuzi na ushirikiano wa utafiti, uimarishaji bora wa kimataifa, athari za kijamii, urahisi wa kufanya biashara, udhibiti wa viwanda, ukubwa wa uwekezaji, athari za usawa wa biashara, uendelevu na majumiano ya ndani.

Michango ya wakala wa uwekezaji katika ushirikiano wa vyuo vikuu na viwanda, ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja, ajira za wanawake, elimu na mengine yaliangaziwa wakati wa tathmini.

Michango ya wakala kwa usambazaji wa ndani

Uwekezaji uliofanywa na michango ya wakala kwa usambazaji wa ugavi wa ndani pia ilikuwa muhimu katika mchakato wa tathmini na uchumi wa nchi, elimu ya vyuo vikuu, uhamishaji wa teknolojia, na "kutoakua na uzalishaji wa kabuni".

Tuzo hiyo ilionekana kama ushahidi wa uwezo wa Uturuki kuvutia uwekezaji na uvumbuzi katika nyanja ya kimataifa.

Mwaka jana, Ofisi ya Uwekezaji ya Uturuki ilipokea tuzo ya Umoja wa Mataifa kwa uwekezaji wake katika mradi wa Yeka-2 unaoendeshwa na kampuni ya huduma za umeme ya Enerjisa yenye makao yake makuu Istanbul.

"Juhudi zetu za kukuza uwezo wa Uturuki katika uwekezaji kwa kiwango cha kimataifa, inayofuatana na dira ya Karne ya Uwekezaji inayoongozwa na rais wetu, zinaendelea kutoa matokeo," alisema A. Burak Daglioglu, rais wa Ofisi ya Uwekezaji ya Uturuki, katika taarifa.

"Tunalenga kuongezekoa kwa sehemu ya nchi yetu ya uwekezaji wa kimataifa kutoka asilimia 1 hadi asilimia 1.5," aliongeza.

TRT World