| swahili
UTURUKI
3 dk kusoma
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Rais wa Uturuki Erdogan amehuzunishwa na tukio hilo, akisema kuwa jitihada za uokozi zinaendelea kwa uratibu wa ndani.
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Ndege hiyo ilipata ajali karibu na mpaka wa Georgia na Azerbaijan ilikuwa na watu 20 raia wa Uturuki, wakati ikitokea Azerbaijan kuelekea Uturuki.
11 Novemba 2025

Wizara ya Mambo ya Ulinzi ya Uturuki imesema siku ya Jumanne kuwa ndege ya Uturuki iliyopata ajali karibu na mpaka wa Georgia na Azerbaijan ilikuwa na watu 20 raia wa Uturuki, wakati ikitokea Azerbaijan kuelekea Uturuki.

Katika taarifa yake ya awali, wizara hiyo ilisema kuwa ndege hiyo ilitoka Azerbaijan kuja nchini kwetu kabla haijapata ajali kwenye mpaka wa Georgia na Azerbaijan,” ikiongeza kuwa shughuli za uokozi zinaendelea chini ya uratibu wa mamlaka za Azerbaijan na Georgia.

Hakuna taarifa zozote zilizotolewa kuhusu vifo au majeruhi wa tukio hilo.

Rais Recep Tayyip Erdogan alisema kuwa alihuzunishwa sana na tukio hilo, akiongeza kuwa shughuli za kufikia eneo hilo zinaendelea.

“Kazi yetu inaendelea chini ya uratibu wa mamlaka husika. Mungu awarehemu mashahidi wetu,” alisema Erdogan kupitia mtandao wa X.

Kulingana na wizara hiyo, uchunguzi wa kujua chanzo cha tukio hilo umeanza.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uturuki Ali Yerlikaya alisikitishwa na tukio hilo kupitia mtandao wa wa kijamii wa NSosyal.

Yerlikaya alisema kuwa alijadiliana kuhusu tukio hilo kwa njia ya simu na mwenzake wa Georgia Gela Geladze, ambaye alisema alikuwa anaelekea eneo la tukio.

Kupitia mtandao wa NSosyal, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Uturuki Burhanettin Duran alisema kuwa shughuli ya uokozi na utafutaji ilikuwa inaendelea kwa kasi.

“Ili kuhakikisha kuwa tuna taarifa sahihi, tunatoa wito kwa umma kuamini tu taarifa zinazotolewa na mamlaka rasmi na kupuuzia taarifa potofu,” aliongeza.

Jitihada za uokozi za Georgia

Kulingana na vyanzo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan alikuwa na mazungumzo ya simu na mwenzake wa Georgia, Maka Botchorishvili, kuzungumzia jitihada za uokozi.

Botchorishvili pia alituma salamu zake za rambirambi kufuatia ajali hiyo.

Kwa upande wake, mamlaka ya usalama wa anga ya Georgia Sakaeronavigatsia ilisema kuwa ndege hiyo ilipata ajali karibu na mpaka na Azerbaijan.

Katika taarifa yake kwenye mtandao wa Facebook, mamlaka hiyo ilisema kuwa ndege hiyo ilipotea kutoka kwenye rada, dakika chache baada ya kuvuka eneo la Georgia bila kutuma ujumbe wowote.

Rambirambi kutoka Azerbaijan

Kufuatia tukio, Rais wa Azarbaijan Ilham Aliyev alikuwa na mazungumzo ya simu na mwenzake wa Uturuki na kutuma salamu zake za rambirambi kufuatia tukio hilo.

"Wakati wa mazungumzo hayo, ilitaarifiwa kuwa mamlaka za Azerbaijan na Uturuki walikuwa pamoja kushughulikia tukio hilo," ilisema taarifa hiyo.

Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Uturuki Cevdet Yilmaz alikuwa na mazungumzo na Waziri na Waziri Mkuu wa Azerbaijan Ali Asadov, kuhusu tukio hilo.

Kupitia ukurasa wa NSosyal, Yilmaz alisema kuwa Asadov alituma salamu za rambirambi kutoka Azerbaijan na kusisitiza kuwa nchi hiyo inafuatilia hali hiyo.

Yilmaz alimshukuru kiongozi wa Azerbaijan kwa sala na matashi yake.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Uturuki inaangazia ushirikiano na ujumuishi katika nia ya kuandaa mkutano wa COP31
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan