| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Mabaki ya miili ya wanajeshi hao yamepelekwa nyumbani kwao baada ya hafla hiyo.
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Hafla hiyo ilijumuisha kutoa heshima, kusomewa Qur'ani Tukufu na maombi kwa ajili ya askari waliokufa. /
14 Novemba 2025

Hafla ya kuwaaga wanajeshi wa Uturuki waliopoteza maisha kwenye ajali ya hivi karibuni ya ndege ya kijeshi ilifanyika Ijumaa katika Kituo cha Jeshi la Anga cha Murted, jijini Ankara.

Ndege ya Jeshi la Anga la Uturuki aina ya C-130 ilianguka karibu na mpaka wa Azerbaijan na Georgia tarehe 11 Novemba, na kusababisha vifo vya watu wote 20 waliokuwa ndani ya ndege hiyo.

Hafla hiyo ilijumuisha kusimama kimya kwa dakika moja, kusomwa kwa Qur’ani Tukufu na dua kwa ajili ya wanajeshi waliopoteza maisha.

Baada ya kusomwa kwa taarifa za utambulisho wa kila mwanajeshi, majeneza yao yalibebwa na kupelekwa kwenye ndege za kijeshi kwa ajili ya kusafirishwa hadi nyumbani kwao kwa ajili ya kuzikwa. 

Miongoni mwa walioudhuria sherehe hiyo ni Spika wa Bunge Numan Kurtulmuş, Waziri wa Ulinzi wa Taifa Yaşar Güler, Waziri wa Familia na Huduma za Jamii Mahinur Özdemir Göktaş, wabunge, makamanda wakuu wa Jeshi la Uturuki, Mkuu wa Mkoa wa Ankara Vasip Şahin, Kamanda wa Jeshi la Anga la Azerbaijan Meja Jenerali Namig Islamzade, Balozi wa Azerbaijan nchini Ankara Reshad Mammadov, pamoja na familia za wanajeshi hao.

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan alitoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu, akieleza huzuni yake kubwa kutokana na msiba huo na kuwaombea faraja na nguvu katika kipindi hiki kigumu.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki inaangazia ushirikiano na ujumuishi katika nia ya kuandaa mkutano wa COP31
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan