| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameonesha mshikamano na Waturuki wa Ahiska, akisema kuwa machungu ya Wahiska 100,000 bado yanaendelea.
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.
14 Novemba 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, siku ya Ijumaa aliadhimisha kumbukumbu ya miaka 81 ya kuwa uhamishoni kwa Waturuki Wahiska kutoka katika eneo la (Akhaltsikhe/Meskheti) nchini Georgia, na vifo vyao mwaka 1944.

“Mioyoni mwetu bado tuna uchungu wa watu wapatao laki moja walioondolewa kutoka ardhi yao ya asili Novemba 14, 1944,” alisema Erdogan kwenye mtandao wa kijamii wa Uturuki wa NSosyal.

Aliwaombea watu hao huruma ya Mungu, akiongeza kuwa bado ana maumivu ya waliyopitia Waturuki Wahiska kwenye kumbukumbu ya miaka 81.

Katika taarifa yake, Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki ilisema kuwa, mnamo Novemba 14, watu wapatao 100,000 waliondolewa kutoka kwenye maeneo yao katika eneo la Ahiska ndani ya jamhuri iliyokuwa ya Kisovietu ya Georgia, yenye kupakana na Uturuki na kupelekwa kwenye maeneo ya ndani zaidi.

Maelfu ya watu walipoteza maisha kwa njaa, baridi na magonjwa kwenye safari hiyo ya mateso, taarifa hiyo iliongeza.

“Kwenye kumbukumbu hii ya miaka 81, tunakumbuka kwa masikitiko makubwa janga hili kubwa na kwa heshima zote tunawakumbuka ndugu zetu waliopteza maisha wakiwa uhamishoni,” ilisema taarifa hiyo.

Iliongeza kuwa, licha ya mates ohayo, watu hao waliweza kuhifadhi utambulisho wao, lugha, imani na kufanikiwa kurithisha kwa vizazi vingine.

Kwa upande mwingine, Uturuki imesema kuwa inatumai kuwa mchakato wa wa kuwawezesha Waturuki Meskhetian kurejea kwenye makazi yao ya asili, utakuwa wa mafanikio.

Uhamisho wa 1944

Mnamo Novemba 14, 1944, mamlaka za Kisovieti, ziliwatuhumu wakazi wa Akhaltsikhe, ambao ni mji mkuu wa mkoa wa Meskheti, kuhusika na tishio la amani.

Ndani ya saa chache, zaidi ya watu 90,000, wakiwemo wanawake, watoto na wazee waliondolewa kwenye nyumba zao na kupakiwa kwenye magari ya mizigo.

Watu hao walisafirishwa kwa mwezi mmoja kuelekea maeneo ya kati ya Asia, huku 17, 000 kati ya hao, wakipoteza maisha kutokana na njaa, baridi na magonjwa.

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Uturuki inaangazia ushirikiano na ujumuishi katika nia ya kuandaa mkutano wa COP31
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan