| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Rais wa Uturuki amemuenzi mwanzilishi huyo wa jamhuri akitangaza ufunguzi wa eneo alilozaliwa Ataturk.
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Ataturk aliongoza mapambano ya Uturuki ya kudai uhuru pamoja na kuanzisha jamhuri mwaka 1923.
10 Novemba 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumatatu, aliongoza adhimisho la miaka 87 ya kifo cha Mustafa Kemal Ataturk, baba wa taifa na mwanzilishi wa jamhuri ya Uturuki.

Akizungumza wakati wa adhimisho hilo, Erdogan alimuenzi Ataturk, akiwashukuru wanachama wa kwanza wa Bunge la Taifa, ambao waliongoza mapambano ya uhuru na uanzishwaji wa dola mpya ya Uturuki.

Pia, alitoa heshima kwenye kumbukumbu ya mashahidi wa taifa—wakiwemo wale wa ukombozi wa Istanbul na mapambano ya Canakkale na mashujaa wa Julai 15 ambao walizima jaribio la mapinduzi.

Akinukuu kauli maarufu ya Ataturk, “Siku  moja, mwili wangu utageuka kuwa mavumbi, lakini Jamhuri ya Uturuki itaendelea kuwepo,” Erdogan alisema kauli hiyo inasadifu maono ya mwanzilishi kwa ajili ya taifa imara.

 “Kumuenzi Ataturk inamaanisha kuimarisha jamhuri yetu na kuifanya iwe ya mafanikio katika kila nyanja,” alisema Rais Erdogan.

Ugiriki, alikozaliwa Ataturk

Katika hatua nyingine, Erdogan alitangaza kukamilika kwa ukarabati wa miezi 11 wa eneo alilozaliwa Ataturk huko Thessaloniki nchini Ugiriki, mchakato uliotaribiwa na Wizara ya Utalii na Utamaduni na Shirika la Maendeleo la Uturuki (TIKA).

“Eneo hili la kihistoria limekarabatiwa na sasa liko wazi kwa wageni na watalii,” alisema Erdogan, akielezea mradi huo kuwa ni sehemi ya jitihada za kuhifadhi urithi wa Ataturk.

Ataturk, ambaye aliongoza mapambano ya Uturuki ya kudai uhuru pamoja na kuanzisha jamhuri mwaka 1923, alifariki dunia Novemba 10, 1938, akiwa na umri wa miaka 57, ndani ya kasri ya Dolmabahce jijini Istanbul.

Kila mwaka, ifikapo saa 9 na dakika 5 asubuhi, taifa humkumbuka kiongozi huyo, likienzi mchango wake katika nchi hiyo.

 

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
Uturuki inaangazia ushirikiano na ujumuishi katika nia ya kuandaa mkutano wa COP31
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan