tokea masaa 13
Aliyekuwa waziri mkuu wa Ufaransa, Lionel Jospin, amefariki dunia.
Kulingana na familia yake, Jospin ambaye anakumbukwa na utaratibu wa kuanzisha ufanyaji kazi saa 35 kwa wiki, amefariki dunia siku ya Jumapili, akiwa na umri wa miaka 88.
Jospin aliiongoza nchi hiyo kati ya mwaka 1997 na 2002, kabla ya kupoteza kwa wanasiasa wa mrengo wa kulia.
Aligombea kiti cha urais mwaka 2002, dhidi ya Jacques Chirac.
CHANZO:AFP















