| swahili
UTURUKI
4 dk kusoma
Harakati za Zero Waste za Uturuki zinaadhimisha mwaka wa 8 wa athari za kiuchumi, kimazingira
Juhudi za Mke wa Kwanza wa Uturuki Emine Erdogan zinathibitisha kuwa mfano wa kuwajibika kwa mazingira, ufanisi wa kiuchumi, na ushirikiano wa kimataifa, huku zikionyesha jinsi hatua za ndani zinavyoweza kuleta mabadiliko duniani kote.
Harakati za Zero Waste za Uturuki zinaadhimisha mwaka wa 8 wa athari za kiuchumi, kimazingira
Mradi umekua na kuwa mpango wa kimataifa wa kukuza ufanisi wa rasilimali, upunguzaji wa taka, na uhamasishaji wa umma.
27 Septemba 2025

Harakati za sifuri taka nchini Uturuki, zinazoongozwa na Mama wa Taifa Emine Erdogan, zinaadhimisha miaka minane mwaka huu, zikionyesha dhamira ya nchi hiyo kwa uendelevu na utunzaji wa mazingira.

Mradi huu ulianzishwa tarehe 27 Septemba 2017 chini ya uangalizi wa Erdogan, na umekua kuwa mpango wa kimataifa wa mazingira unaopigia debe matumizi bora ya rasilimali, kupunguza taka, na kuongeza uelewa wa umma.

Kwa kaulimbiu "Miaka 8 kwa Watu Bilioni 8," harakati hii inaendelea kupanuka kupitia kampeni za mitandao ya kijamii. Ikiwa chini ya uratibu wa Wizara ya Mazingira, Mjini na Mabadiliko ya Tabianchi, mpango huu umeleta matokeo makubwa katika uhifadhi wa nishati, kupunguza gesi chafu, usimamizi wa taka, na akiba ya kiuchumi.

Katika kipindi cha miaka minane, mradi huu umeanzisha mifumo ya usimamizi wa sifuri taka katika majengo 205,000, na kuongeza kiwango cha kitaifa cha kuchakata taka kutoka asilimia 13 mwaka 2017 hadi asilimia 36.08 mwaka 2024, huku lengo likiwa kufikia asilimia 60 ifikapo mwaka 2035.

Takriban tani milioni 74.5 za vifaa vinavyoweza kuchakatwa, ikiwa ni pamoja na karatasi, plastiki, glasi, metali, na taka za kikaboni, zimekusanywa, na kuchangia Lira bilioni 256 katika uchumi wa Uturuki.

Mpango huu pia umezuia ukataji wa miti milioni 552.7, kuokoa lita trilioni 1.71 za maji, lita bilioni 54.6 za mafuta, na kilowati-saa bilioni 227.3 za nishati, huku ukiepuka tani milioni 150 za utoaji wa gesi ya kaboni dioksidi.

Sehemu ya baharini ya harakati hii, Zero Waste Blue, iliyoanzishwa tarehe 10 Juni 2019, imeondoa takriban tani 585,000 za taka za baharini kutoka pwani za Uturuki. Mradi huu pia unajumuisha mfumo wa kurudisha chupa, ambao kwa sasa unakusanya chupa za vinywaji 50,000 kila siku, huku mipango ikiwa ya kupanua mfumo huu kitaifa.

Juhudi za Uturuki zapata kutambuliwa kimataifa

Juhudi za sifuri taka za Uturuki zimepata sifa kimataifa. Mnamo Desemba 2022, Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa ulitangaza tarehe 30 Machi kuwa "Siku ya Kimataifa ya Sifuri Taka."

Emine Erdogan alikua mke wa kwanza wa kiongozi wa Kituruki kuhutubia Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika kikao maalum cha sifuri taka, ambapo Bodi ya Ushauri ya Juu ya Sifuri Taka ilianzishwa chini ya uongozi wake.

Wakati wa Mkutano Mkuu wa 78 wa Umoja wa Mataifa, Uturuki iliandaa tukio la “Kuelekea Harakati ya Kimataifa ya Sifuri Taka” katika Nyumba ya Uturuki (Turkevi), ambapo Rais Recep Tayyip Erdogan alikua wa kwanza kusaini Tamko la Wema wa Sifuri Taka Duniani, lililoanzishwa na Emine Erdogan.

Tangu kuzinduliwa, jukwaa la mtandaoni limevutia zaidi ya wanaharakati wa sifuri taka 15,000 kutoka nchi 114.

Zaidi ya wake wa viongozi wa dunia 50, wawakilishi wa ngazi za juu wa mashirika ya kimataifa, na mawaziri wa mambo ya nje pia wameunga mkono tamko hilo, likionyesha kufikia kwa harakati hii kimataifa.

Hivi karibuni, katika Mkutano Mkuu wa 80, Emine Erdogan alikutana na Zita Oligui Nguema, mke wa Rais wa Gabon Brice Clotaire Oligui Nguema, ambaye alionyesha nia ya kupitisha mfano wa sifuri taka wa Uturuki na kushirikiana katika miradi ya uendelevu.

Erdogan alithibitisha kuwa Taasisi ya Sifuri Taka inaweza kutoa mafunzo ya kiufundi na msaada kuwezesha utekelezaji wa programu hiyo nchini Gabon.

Mpango huu pia umetambuliwa katika majukwaa mengine ya kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuidhinishwa kwa Tamko la Wema wa Sifuri Taka Duniani na nchi wanachama wa G20 wakati wa urais wa India mwaka 2023.

Uongozi wa Emine Erdogan umepatia mradi huu tuzo nyingi za kimataifa, ikiwa ni pamoja na Tuzo ya FAO “Zero Hunger, Zero Waste” (2018), Tuzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya UNDP (2021), Tuzo ya UN-Habitat Waste Wise Cities Global Champion (2021), Tuzo ya Bunge la Mediterania (2022), na Tuzo ya Uongozi wa Hali ya Hewa na Maendeleo ya Benki ya Dunia (2022).

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi