| swahili
UTURUKI
1 dk kusoma
Erdogan kuhusu UNGA: Suala la Palestina lilitawala, Israel ilisahaulika, kikao na Trump kinatia moyo
Hakuna aliye tayari kusimama na Israel au kuonekana kwenye picha na serikali ya Netanyahu, isipokuwa mataifa machache,' anasema Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan.
Erdogan kuhusu UNGA: Suala la Palestina lilitawala, Israel ilisahaulika, kikao na Trump kinatia moyo
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan./Picha:AA
29 Septemba 2025

Rais wa Uturuki aliweka msisitizo kwenye umuhimu wa vuguvugu la Palestina wakati wa kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York, akisema, “pamoja na jitihada za kulizuia,  vuguvugu hilo limeacha alama katika mkutano huo wa 80."

“Hakuna aliye tayari kusimama na Israel au kuonekana kwenye picha na serikali ya Netanyahu, isipokuwa mataifa machache," alisema Recep Tayyip Erdogan katika hutoba yake kwa taifa baada ya kikao cha baraza la mawaziri.

Akipongeza orodha ya nchi zilizoitambua Palestina ambazo zimefikia 158, Erdogan alisema kuwa "tunafarajika sana kama taifa lenye kuongoza mapambano haya."

Kulingana na Erdogan, Uturuki inasimama na Wapalestina katika kulinda ardhi, uhuru na utu wao.

"Licha ya kucheleweshwa, utambuzi wa dola ya Palestina na wajumbe wawili wa baraza la usalama ni jambo muhimu sana,” aliongeza.

" Walau kila mtu anakubali kuwa Netanyahu anachochea vurugu za ulimwengu na kikanda akibakia madarakani huku kukiwa na uchunguzi wa ufisadi," alisema Erdogan.

Akizungumzia kikao chake cha wiki iliyopita alichofanya na Rais wa Marekani Trump, Rais Erdogan alisema: "Nina imani kuwa tutaona matokeo chanya ya mkutano huo katika siku zijazo.”

 

CHANZO:Anadolu Agency
Soma zaidi
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi