8 Januari 2026
Ishara hiyo ilitafsiriwa na mashabiki wengi kuwa ya kudhalilisha. Amoura amesema hakujua maana halisi ya ishara hiyo na anasikitishwa na sintofahamu iliyojitokeza.Mashabiki wengi waliitafsiri ishara hiyo kama kejeli dhidi ya Michel Nkuka Mboladinga, shabiki wa DRC almaarufu “Lumumba Vea.”
“Nilikua na hisia kali sana wakati huo na sikujua umuhimu wa yule mtu aliyekuwa jukwaani. Naomba radhi kwa mashabiki wa Congo,” Amoura aliandika katika ukurasa wake wa Instagram.
ZILIZOPENDEKEZWA
“Ninaiheshimu Congo na timu yao. Kwa dhati kabisa nawatakia kila la heri na natumaini watafanikiwa kufuzu Kombe la Dunia. Ikiwa tabia yangu ilieleweka vibaya, naomba radhi kwa moyo wote kwa sababu haikuwa dhamira yangu hata kidogo,” alisema.
CHANZO:TRT Afrika


















