| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika (CDC) kimesema bara hilo linakabiliwa na mlipuko mbaya zaidi wa kipindupindu katika kipindi cha robo karne, hali inayochochewa na mifumo dhaifu ya maji na migogoro.
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Takriban visa 300,000 vya kipindupindu vimesajiliwa barani Afrika katika siku za hivi karibuni. /
14 Novemba 2025

Takwimu zinaonyesha maambukizi takriban 300,000 ya kipindupindu na zaidi ya vifo 7,000, ongezeko la zaidi ya asilimia 30 kutoka mwaka uliopita.

Nchi za Angola na Burundi zimerekodi ongezeko kubwa la maambukizi kutokana na upatikanaji mdogo wa maji safi.

Hata hivyo, kituo hicho kimesema mlipuko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unaonekana kudhibitiwa, ingawa maeneo yenye migogoro bado yako hatarini, huku ugonjwa huo ukienea kwa haraka katika kambi zilizojaa watu na usafi duni.

Hata hivyo hali imeimarika katika nchi za Sudan Kusini na Somalia.

CDC ya Afrika ilisema kuwa Ethiopia imegundua watu wanane wanaoshukiwa kuwa na homa ya kuambukiza na inasubiri matokeo ili kubaini sababu haswa ya ugonjwa huo.

Aidha CDC ya Afrika ilisema mlipuko wa Mpox unapungua katika baadhi ya maeneo yaliyoathiriwa zaidi lakini bado ni wasiwasi katika maeneo kama Kenya, Guinea, Liberia na Ghana.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi