| swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Shirika la YTB laorodhesha mafanikio ya Afrika mwaka 2024 katika kitabu chao
Shirika linalohudumia Waturuki wanaoishi Ughaibuni na Jamii Husika (YTB) limezindua kitabu chao cha Afrika 2024 ili kuonesha matukio muhimu yaliyotokea katika bara la Afrika.
Shirika la YTB laorodhesha mafanikio ya Afrika mwaka 2024  katika kitabu chao
Kwa jumla, ina nakala 12 za kitaasisi, zilizoandikwa na waandishi 53.
17 Novemba 2025

Ofisi ya Mwenyekiti wa Shirika linlaohudumia Waturuki wanaoishi Ughaibuni na Jamii Husika (YTB) imezindua Kitabu cha Mwaka cha Afrika 2024, toleo jipya kabisa la uchapishaji wake wa kila mwaka linaoangazia maendeleo katika bara la Afrika.

Kwa mujibu wa taarifa ya YTB, kitabu hicho ni tathmini ya kila mwaka ya Uturuki kuhusu Afrika, ikitoa muhtasari wa kina na wa kimfumo kuhusu maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, kijeshi, kiteknolojia, kimazingira na kijamii barani humo.

Kitabu hicho, ambacho kilichapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 2022 na kinapatikana kwa lugha ya Kituruki na Kiingereza, pia kinamulika ajenda chanya katika bara la Afrika, zikiwemo hatua zilizopigwa katika elimu, utamaduni, sanaa, michezo, sinema na muziki.

Toleo la mwaka huu lina vipengele vitano vikuu: Siasa, Uchumi, Jamii na Mazingira; Mahusiano ya Uturuki na Afrika; Mahusiano ya Wadau wa Kikanda, Kimataifa na Afrika; Utamaduni, Sanaa, Elimu na Michezo; pamoja na machapisho kuhusu Afrika.

Athari za kimataifa

Kitabu hiki pia kinajadili matukio yenye athari kubwa duniani, ikiwemo utatuzi wa mgogoro kati ya Somalia na Ethiopia kupitia usuluhishi wa Uturuki mwaka 2024, pamoja na kesi ya mauaji ya halaiki iliyofunguliwa dhidi ya Israel na nchi ya Afrika Kusini.

Kwa jumla, kitabu hichi kina makala 12 za kitaasisi na michango kutoka kwa waandishi 53, ikiweka pamoja jumla ya makala 66 na tathmini ya vitabu 9. Toleo hili linaanza na dibaji iliyoandikwa na Emine Erdoğan, mke wa rais wa Uturuki.

YTB inaeleza kuwa kitabu hiki kina lengo la kuwezesha tathmini ya kina na ya kimkakati kuhusu mahusiano kati ya Uturuki na Afrika.

Miongoni mwa wachangiaji ni taasisi kuu za kitaifa kama Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Ulinzi, Ofisi ya Masuala ya Kidini, Taasisi ya Yunus Emre (YEE), Shirika la Ushirikiano na Uratibu la Uturuki (TİKA), Taasisi ya Maarif, Shirika la Hilali Nyekundu la Uturuku, Shirika la Habari la Anadolu, Shirika la Utangazaji la TRT, Baraza la Mahusiano ya Kiuchumi ya Nje (DEİK), na Shirika la Ndege la Uturuki.

Mbali na uchambuzi wa kisekta, chapisho hili linaangazia pia matukio ya kimataifa yenye athari kubwa kwa Afrika, yakiwemo usuluhishi uliofanywa na Uturuki uliosaidia kupunguza mvutano kati ya Somalia na Ethiopia mwaka 2024, pamoja na kesi ya mauaji ya halaiki iliyofunguliwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel.

Soma zaidi
Uturuki inakaribisha makubaliano ya amani kati ya serikali ya DRC na waasi wa M23
Uungwaji mkono wa Ujerumani unaashiria 'upya wa nia ya kisiasa' kwa ombi la Uturuki la EU: Fidan
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan