| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Serikali ya DRC ilitoa hati yake ya kukamatwa kwake mwaka 2011 baada ya kuhusishwa na kukiunga mkono kikundi cha waasi cha M23, na kulazimika kukimbilia nchini Ufaransa.
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Lumbala anashitakiwa kwa kushiriki uhalifu dhidi ya binadamu, wakati wa mgogoro wa kisiasa kati yam waka 1998 na 2008, nchini DRC./Picha:Wengine
12 Novemba 2025

Shauri linalomkabili kiongozi wa zamani wa waasi nchini DRC Roger Lumbala, limeanza kusikilizwa jijini Paris.

Lumbala anashitakiwa kwa kushiriki uhalifu dhidi ya binadamu, wakati wa mgogoro wa kisiasa kati yam waka 1998 na 2008, nchini DRC.

Kiongozi huyo wa waasi anakabiliwa na kifungo cha maisha gerezani, hukumu ambayo inatarajiwa kutolewa Disemba 19.

Lumbala, mwenye umri wa miaka 67, aliongoza kikundi cha waasi kiitwacho Congolese Rally for National Democracy, kilichokuwa kikiungwa mkono na Uganda, kikituhumiwa kwa kutesa raia, hususani wale kutoka jamii za Nande na Mambuti.

Kulingana na Umoja wa Mataifa, kikundi hicho kilitesa watu pamoja na kufanya vitendo vya ubakaji.

Baada ya vita hivyo, Lumbala alihudumu kama Waziri wa Biashara ya Nje, katika serikali ya mpito ya DRC, kati ya mwaka 2003 na 2005 kabla hajateuliwa kuwa mbunge.

Serikali ya DRC ilitoa hati yake ya kukamatwa kwake mwaka 2011 baada ya kuhusishwa na kukiunga mkono kikundi cha waasi cha M23, na kulazimika kukimbilia nchini Ufaransa.

CHANZO:AP
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano