AFRIKA
1 dk kusoma
Viongozi wa Dunia wakutana Beijing kwa kongamano la kuwawezesha Wanawake
Rais wa China Xi Jinping na mkewe Peng Liyuan wamefungua rasmi mkutano wa Viongozi wa Dunia kuhusu Wanawake kwa kujumuika pamoja na viongozi kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni.
Viongozi wa Dunia wakutana Beijing kwa kongamano la kuwawezesha Wanawake
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina Mohammed. / Reuters
tokea masaa 13

Kongamano hilo linawaleta pamoja viongozi wa nchi, waasisi wa biashara, wavumbuzi wa teknolojia, na mabalozi wa utamaduni —wakiangazia mikakati ya kuimarisha maisha na kuwawezesha wanawake.

Baadhi ya vikao muhimu vitaangazia mifumo ya kidijitali, ujasiriamali, na mifumo ya sera ambayo itaimarisha nafasi ya wanawake katika ngazi za uongozi.

Kwa viongozi vijana duniani na wajasiriamali wenye nia ya kufaidi masoko yanayoibuka, mkutano huu utakuwa ukiangazia fursa hizo pia.

Watoa mada wataonesha data za namna teknolojia inaweza kusaidia wanawake kuanzisha biashara na kuwa sehemu ya maendeleo ya uchumi.

Pia masuala kama ya haki za binadamu, upatikanaji sawa wa elimu kwa wote na namna sanaa na michezo inaweza kusaidia ukuzaji.

Watoa mada pia wataangazia namna hayo yote yatakavyoweza kusaidia kupazwa kwa sauti za wanawake kupitia tamaduni mbalimbali.

CHANZO:TRT Afrika Swahili