| swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Rais wa Marekani Trump anapongeza "siku kubwa kwa Mashariki ya Kati" wakati yeye na viongozi wa eneo hilo wakitia saini azimio la kusitisha mapigano Gaza baada ya mabadilishano ya wafungwa wa Israel na Hamas.
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Uturuki, Misri, Qatar na Marekani zatia saini hati ya kusitisha mapigano Gaza. /
13 Oktoba 2025

Misri, Qatar na Uturuki zimetia saini pamoja na Rais wa Marekani Donald Trump hati ya makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza.

Hati hiyo ilisainiwa siku ya Jumatatu wakati wa mkutano wa kimataifa ulioandaliwa na Misri katika mji wa Sharm el-Sheikh.

Trump alipongeza "siku kubwa kwa Mashariki ya Kati" wakati yeye na viongozi wa eneo hilo walitia saini azimio lililokusudiwa kusisitiza usitishaji vita huko Gaza, saa chache baada ya Israel na Hamas kubadilishana mateka na wafungwa.

"Hii ni siku kubwa sana kwa ulimwengu, ni siku kubwa sana kwa Mashariki ya Kati," Trump alisema huku zaidi ya viongozi kumi na wawili wa dunia walikutana kuzungumza katika mkutano huo.

"Waraka huo utaelezea sheria na kanuni na mambo mengine mengi," Trump alisema kabla ya kutia saini, akirudia mara mbili kwamba "makubalioano ya kusitisha vita yatafanikiwa."

Mkutano wa ujenzi wa Gaza

Rais wa Misri Abdel Fattah el Sisi alisema kuwa nchi yake itaandaa mkutano kuhusu ujenzi mpya wa Gaza kufuatia makubaliano ya kusitisha mapigano na kubadilishana wafungwa na mateka.

"Misri itafanya kazi na Marekani kwa uratibu na washirika katika siku zijazo ili kuweka msingi wa ujenzi wa Gaza, na tunakusudia kuandaa mkutano wa mapema wa kufufua, kujenga na maendeleo," alisema.

Sisi pia alisema kuwa mkataba wa Gaza "unafunga wakati mgumu katika historia ya mwanadamu na kufungua enzi mpya ya amani na utulivu" kwa Mashariki ya Kati.

Aliongeza kuwa iliadhimisha "siku ya kihistoria" ya amani ambayo iliweka msingi wa suluhisho la serikali mbili.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Israel yafanya mashambulizi ya anga dhidi ya Gaza na kukiuka makubaliano ya kusitisha vita
Malkia wa zamani wa Thailand Sirikit afariki dunia akiwa na umri 93
Maseneta wa Marekani wanamtaka Trump kuchukua msimamo thabiti dhidi ya unyakuzi wa West Bank
Waziri Mkuu wa Israel amfuta kazi msaidizi wake mkuu wa usalama kwa mtafaruku juu ya Gaza
Mbu wapatikana nchini Iceland kwa mara ya kwanza
Kiongozi Mkuu wa Iran, Khamenei, apinga madai kuwa Marekani imeharibu uwezo wa nyuklia wa nchi yake
Mashambulizi mapya ya Israel yawauwa takriban Wapalestina 21 huko Gaza licha ya kusitishwa kwa vita
Gaza inaishutumu Israel kwa wizi wa viungo kutoka kwa Wapalestina, inataka uchunguzi wa kimataifa
ICC inakataa ombi la Israel la kukata rufaa kuhusu vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na Gallant
Israel yapunguza upatikanaji wa misaada kwa nusu, inazuia mafuta kuingia Gaza
Mabomu ambayo hayajalipuka yana hatari 'kubwa' huko Gaza, NGO yaonya
Marekani katika kizungumkuti cha kutumia dhahabu yake kulipia deni la taifa
'Sura mpya kwa amani' — Dunia inajibu baada ya kusaini hati rasmi ya kumaliza vita vya Gaza
Kuachiliwa kwa mateka kutaanza Gaza saa 11 alfajiri, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti
Israel inadhulumu wafungwa Wapalestina kabla ya kuachiliwa chini ya makubaliano na Hamas, video inaonyesha
Trump, Sisi kushirikiana kuandaa mkutano wa Gaza huko Sharm el-Sheikh nchini Misri
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2025
Wapalestina 200,000 wanarejea kaskazini mwa Gaza huku wanajeshi wa Israel wakiondoka
Wanajeshi wa Marekani wawasili Israel kusaidia kufuatilia usitishaji mapigano Gaza
Trump ataungana na viongozi, wanadiplomasia kutoka Uturuki na wengine kwenye mkutano wa Gaza, Cairo