tokea masaa 4
Timu hiyo kutoka visiwa vilivyo kando ya pwani ya Senegal ina idadi ya watu wapatao 550,000, na hivyo kuifanya Cape Verde kuwa nchi yenye idadi ndogo zaidi ya watu kuwahi kuiwakilisha Afrika kwenye fainali za Kombe la Dunia.
Cape Verde inaongoza Kundi D kwa alama 23, alama nne zaidi ya Cameroon waliomaliza nafasi ya pili.
Cameroon, ambao wanashikilia rekodi ya Afrika kwa kushiriki Kombe la Dunia mara nyingi zaidi (mara 8 ), walitoka sare ya 0-0 dhidi ya Angola mjini Yaoundé, Cameroon.
CHANZO:TRT Afrika, AFP