AFRIKA
1 dk kusoma
Cape Verde yaandika historia kwa kufuzu Kombe la Dunia 2026 kwa mara ya kwanza
Cape Verde iliichapa Eswatini mabao 3-0 siku ya Jumatatu na kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026, hatua inayoiwezesha kushiriki mashindano hayo ya kimataifa kwa mara ya kwanza kabisa katika historia ya taifa hilo.
Cape Verde yaandika historia kwa kufuzu Kombe la Dunia 2026 kwa mara ya kwanza
Timu ya taifa ya kandanda ya Cape Verde imefuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo. / / Wengine
tokea masaa 4

Timu hiyo kutoka visiwa vilivyo kando ya pwani ya Senegal ina idadi ya watu wapatao 550,000, na hivyo kuifanya Cape Verde kuwa nchi yenye idadi ndogo zaidi ya watu kuwahi kuiwakilisha Afrika kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Cape Verde inaongoza Kundi D kwa alama 23, alama nne zaidi ya Cameroon waliomaliza nafasi ya pili.

Cameroon, ambao wanashikilia rekodi ya Afrika kwa kushiriki Kombe la Dunia mara nyingi zaidi (mara 8 ), walitoka sare ya 0-0 dhidi ya Angola mjini Yaoundé, Cameroon.

CHANZO:TRT Afrika, AFP