| swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Kampuni ya Boeing kulipa zaidi ya dola milioni 28 kwa familia ya aliyefariki katika ajali ya ndege
Kama idadi kubwa ya abiria wengine katika ndege hiyo iliyoanguka, Garg, mshauri wa Mipango ya Maendeleo wa Umoja wa Mataifa, alikuwa akielekea kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mazingira huko Nairobi, Kenya.
Kampuni ya Boeing kulipa zaidi ya dola milioni 28 kwa familia ya aliyefariki katika ajali ya ndege
Ndege ya Boeing ilianguka Ethiopia Machi 2018
13 Novemba 2025

Mahakama ya Marekani imeamuru zaidi ya dola milioni 28 ipewe familia ya mshauri wa Umoja wa Mataifa aliyefariki katika ajali ya ndege aina ya Boeing 737 Max nchini Ethiopia zaidi ya miaka sita iliyopita.

Uamuzi huo ulifikiwa Jumatano kwa niaba ya jamaa wa Shikha Garg baada ya saa mbili ya mashauriano ya jopo la wazee wa mahakama (jury) ambayo yalimaliza kesi ya wiki moja huko Chicago, ambapo Boeing ilikuwa na makao yake makuu.

Kama idadi kubwa ya abiria wengine katika ndege hiyo iliyoanguka, Garg, mshauri wa Mipango ya Maendeleo wa Umoja wa Mataifa, alikuwa akielekea kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mazingira huko Nairobi, Kenya.

Ilikuwa ni kesi ya kwanza kwa mtu kudai fidia iliyotokana na ajali ya Machi 2019 ambayo watu wote 157 waliuawa katika ndege ya Ethiopian Airlines 302.

"Sisi na familia tumeridhishwa na uamuzi wa mahakama. Inaelekeza uwajibikaji kwa umma kwa mwenendo mbaya wa Boeing," mawakili wa familia hiyo, Shanin Specter na Elizabeth Crawford, walisema katika taarifa baada ya hukumu hiyo kusomwa mahakamani.

Boeing italipa dola milioni 3.45 za ziada kwa mume wa Garg, Soumya Bhattacharya, kama sehemu ya makubaliano kati yake na kampuni iliyofikiwa nje ya mahakama.

Hiyo, pamoja na malipo ya riba ya 26%, itakuwa jumla ya kiasi ambacho Boeing italipa kwa familia ya Garg hadi $ 35.8 milioni.

Kampuni hiyo ya ndege imejadiliana kuhusu suluhu badala ya kesi mahakamani katika kesi nyingi za vifo zilizowasilishwa kuhusiana na ajali hiyo na nyingine kama hizo ya 737 Max miezi mitano kabla katika pwani ya Indonesia, ingawa maelezo ya makubaliano hayo yalikuwa ya siri na hayakufichuliwa.

Wanasheria wanasema kesi zisizopungua kumi na mbili bado hazijatatuliwa.

Katika taarifa Jumatano, Boeing iliomba msamaha kwa familia zote za waathiriwa na kusema inaheshimu haki yao ya kuwasilisha madai yao mahakamani.


CHANZO:TRT Afrika and agencies
Soma zaidi
Zaidi ya safari za ndege 2,000 zimefutwa nchini Marekani kwa sababu ya kufungwa kwa serikali
Trump ailalamikia Katiba ya Marekani kutomruhusu kuwania muhula wa tatu
Israel yafanya mashambulizi ya anga dhidi ya Gaza na kukiuka makubaliano ya kusitisha vita
Malkia wa zamani wa Thailand Sirikit afariki dunia akiwa na umri 93
Maseneta wa Marekani wanamtaka Trump kuchukua msimamo thabiti dhidi ya unyakuzi wa West Bank
Waziri Mkuu wa Israel amfuta kazi msaidizi wake mkuu wa usalama kwa mtafaruku juu ya Gaza
Mbu wapatikana nchini Iceland kwa mara ya kwanza
Kiongozi Mkuu wa Iran, Khamenei, apinga madai kuwa Marekani imeharibu uwezo wa nyuklia wa nchi yake
Mashambulizi mapya ya Israel yawauwa takriban Wapalestina 21 huko Gaza licha ya kusitishwa kwa vita
Gaza inaishutumu Israel kwa wizi wa viungo kutoka kwa Wapalestina, inataka uchunguzi wa kimataifa
ICC inakataa ombi la Israel la kukata rufaa kuhusu vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na Gallant
Israel yapunguza upatikanaji wa misaada kwa nusu, inazuia mafuta kuingia Gaza
Mabomu ambayo hayajalipuka yana hatari 'kubwa' huko Gaza, NGO yaonya
Marekani katika kizungumkuti cha kutumia dhahabu yake kulipia deni la taifa
'Sura mpya kwa amani' — Dunia inajibu baada ya kusaini hati rasmi ya kumaliza vita vya Gaza
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Kuachiliwa kwa mateka kutaanza Gaza saa 11 alfajiri, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti
Israel inadhulumu wafungwa Wapalestina kabla ya kuachiliwa chini ya makubaliano na Hamas, video inaonyesha
Trump, Sisi kushirikiana kuandaa mkutano wa Gaza huko Sharm el-Sheikh nchini Misri
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2025