| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Rais Salva Kiir hakueleza sababu za kuwatimua maafisa, na ni haki yake, kwa kuwa makubaliano ya amani ya 2018 yanampa mamlaka ya kufanya uteuzi katika ngazi ya kitaifa na kwenye majimbo.
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir. PICHA/ MAKTABA
tokea masaa 17

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amefanya mabadiliko katika baraza lake la mawaziri siku ya Jumatatu, na kumteua makamu wa rais mpya pamoja na kumrejesha kwenye baraza mtoto wa rais muasisi wa nchi hiyo.

Rais aliwafuta kazi mawaziri wanne na gavana, na mkuu wa polisi katika mabadiliko ya hivi karibuni katika baraza.

Katika maagizo kadhaa shirika la habari la serikali la Sudan Kusini (SSBC), James Wani Igga amerejeshwa kama makamu wa rais ambapo alitimuliwa miezi tisa iliopita. Anamrithi Benjamin Bol Mel ambaye alifutwa wiki iliopita.

Wani Igga, mwanasisa mkongwe, pia aliteuliwa tena kuwa naibu mwenyekiti wa kwanza wa chama tawala cha SPLM.

Mabior Garang Mabior amerudi tena kwenye baraza kama waziri wa mazingira. Ni mtoto wa rais wa zamani John Garang, aliyefariki katika ajali ya helikopta 2005.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi