| swahili
AFRIKA
3 dk kusoma
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na rubela
WHO imetangaza kuangamizwa kwa magonjwa ya Surua na Rubela nchini Mauritius, Ushelisheli na Cape Verde, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mafanikio hayo kusini mwa jangwa la Sahara.
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Mnamo 2024, chanjo ya dozi ya kwanza dhidi ya surua na rubela ilifikia 71%, kutoka 67%
tokea masaa 16

Katika mafanikio makubwa ya afya ya umma, Cabo Verde, Mauritius na Seychelles zimeondoa surua na rubela, na kuwa nchi za kwanza kusini mwa Jangwa la Sahara kufikia hatua hii.

Tume ya Shirika la Afya ya kukabiliana na maradhi hayo ilitangaza mafanikio hayo Jumatatu likipongeza kama hatua kubwa kwa Afrika.

Naibu waziri wa Afya nchini Mauritius Anishta Babooram alisema kuwa hii matokeo ya kujitolea kwa taasisi za afya nchini humo lakini mtihani mkubwa ni kuhakikisha hautokei tena maambukizi kutoka nje.

"Kuondoa sio mwisho wa safari. Kudumisha hadhi hii kunahitaji umakini wa mara kwa mara, ugunduzi wa haraka na majibu ya haraka kwa maambukizi yoyote kutoka nje,’’ alisema Waziri Babooram. ‘‘Mauritius inasalia kujitolea kikamilifu kudumisha chanjo ya juu, kuimarisha usalama wa afya kuvuka mpaka na kuimarisha mifumo ya tahadhari ya mapema," aliongeza.

Utoaji chanjo

Nchini Mauritius, hakuna maambukizi ya surua ambavyo vimeripotiwa tangu 2019. Nchi ilijibu mlipuko wa surua wa 2018-2019 kwa juhudi mpya za chanjo na uchunguzi. Kufikia 2024, chanjo ya surua,matumbwitumbwi na rubela katika ngazi ya kitaifa ilifikia 98% kwa kipimo cha kwanza na 96% kwa kipimo cha pili.

Ushelisheli imedumisha chanjo ya zaidi ya 95% kwa dozi ya kwanza na ya pili ya chanjo ya surua kwa zaidi ya miongo miwili, ikisaidiwa na ufuatiliaji wa makini, uthibitisho wa kimaabara na uchunguzi wa afya katika maeneo ya kuingia.

Mlipuko wa mwisho wa surua ulidhibitiwa mnamo 2020. Hakuna kesi ya rubela iliyothibitishwa tangu 2016.

"Juhudi hizi endelevu zimekuwa na changamoto lakini kupitia kwa kujitolea kwa Programu yetu ya upanuzi ya timu ya chanjo tumefanikiwa kuzuia maambukizi ya surua na rubela kwa miongo kadhaa," alisema Marvin Fanny, Waziri wa Afya wa Ushelisheli. "Ninajivunia kutangaza kwamba, Ushelisheli imetangazwa kama isiyo na surua na rubela, mafanikio makubwa kwa taifa letu."

Kuzuia vifo

Nchi nyingine Afrika iliyotangazwa pia kuangamiza Surua na Rubela ni Cape Verde ya Magharibi mwa Afrika.

Tangu mwaka wa 2001, nchi nyingi katika kanda ya Afrika zimetekeleza mikakati ya kudhibiti surua ambayo ni pamoja na kutoa dozi mbili za msingi za chanjo, kufanya kampeni za mara kwa mara za chanjo nyingi, ufuatiliaji wa kina wa magonjwa na uboreshaji wa mwitikio wa milipuko pamoja na utunzaji wa kimatibabu kwa wagonjwa wa surua.

Kati ya 2000 na 2023, juhudi hizi zinakadiriwa kuzuia karibu vifo milioni 21, punguzo la 79% la vifo vinavyokadiriwa kila mwaka katika kipindi hiki.

Kwa miaka mingi, utoaji wa chanjo barani Afrika umeongezeka. Mnamo 2024, chanjo ya dozi ya kwanza ya chanjo ya surua na rubela ilifikia 71%, kutoka 67% mnamo 2022, wakati chanjo ya kipimo cha pili ilipanda kutoka 43% hadi 55% katika kipindi hicho.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi