| swahili
Maoni
AFRIKA
3 dk kusoma
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Muenendo wa sasa duniani hautoi tena suluhu au kuangazia upatikanaji wa haki. Hilo limeonekana Gaza, na kabla ya hapo Bosnia na Rwanda. Sasa, inaonekana tena Sudan.
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Takwimu rasmi zinaonesha kuwa vifo kutokana na mauaji ya kikatili ya Al Fasher ni zaidi ya 2,000
12 Novemba 2025

Na Tunç Demirtaş

Kinachotokea wakayi huu el-Fasher, kwa njia nyingi, ni uhalifu dhidi ya ubinadamu. Kuna ushahidi wa kutosha kuonesha kuwa RSF imehusika na ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.

Ndani ya wiki moja, maelfu ya watu wameuawa kikatili dunia ikitizama. Kwa vyovyote vile, hili ni janga kwa watu.

Na hii siyo mara ya kwanza kwa Sudan kupitia matatizo haya. Kwa miezi kumi na nane iliopita, watu wa el-Fasher tayari wamekuwa katika hali mbaya, wanakufa polepole. Hawakuwa wanapata chakula.

Wakati fulani, walilazimika kula chakula cha wanyama hadi nyama ya tumbili, panya, na paka.

Kuanguka kwa mfumo wa haki duniani na msimamo wa Uturuki wa aina yake

Uturuki, pamoja na mataifa kadhaa, imeanza kuzungumzia suala la kuunga mkono watu wa Sudan dhidi ya ukatili wa RSF. Hili linaashiria mtazamo wa Uturuki wa kuzingatia utu kama sehemu ya sera yake ya mambo ya nje. Kote kwa matatizo yanayokumba kuanzia Sudan hadi Gaza sauti ya Uturuki imekuwa ikiskika kila mara na imekuwa na ujasiri na kutoa muelekeo wa wazi.

Itambulike kuwa Rais Recep Tayyip Erdoğan ni mmoja kati ya viongozi wachache duniani ambayo wameleta suala la madhila ya watu wa Sudan katika mjadala wa kimataifa.

Kwa bahati mbaya, wengine wachache wamefanya hivyo pia. Umoja wa Mataifa, wakati huohuo, imeshindwa kuwajibika ipasavyo. Swali siyo kama jamii ya kimataifa inaweza kuingilia kati, lakini kama inataka kufanya hivyo.

Muenendo wa sasa hautoi tena suluhu au kutekeleza haki. Ilionekana Gaza, na kabla ya hapo Bosnia na Rwanda. Sasa, inafanyika Sudan.

Hakuna hatua ya kuwafanya waliotekeleza ukatili. Kila tukio chanzo chake ni ukosefu wa maadili na mfumo wa dunia wa sasa unaoendekeza mfumo huo hasa.

Umuhimu wa kimkakati wa El-Fasher na masuala ya kujifunza ambayo hayakuzingatiwa

El-Fasher ni mji muhimu wa kimkakati. Ukiangalia ramani utagundua kuwa ni eneo la biashara nyingi, hasa wakati wa vita. Ukiweza kudhibiti njia hizi inamaanisha unaweza kudhibiti njia ya bidhaa.

Ni muhimu kutambua kuwa, eneo lenye utajiri mkubwa wa dhahabu la liko sehemu ya Jebel Amir na Songo. Umuhimu wa El-Fasher siyo kwa ajili ya raslimali zake lakini kwa nafasi yake ya kuunganisha mashariki na magharibi mwa Sudan. Pia ina uwanja wa ndege ambao una umuhimu katika masuala ya operesheni.

Darfur ina miji mikubwa mitano. El-Fasher ndiyo mji mkuu Darfur Kaskazini. Hadi wiki iliopita, mji wa Darfur ulikuwa chini ya udhibiti wa jeshi huku wapiganaji wa RSF tayari walikuwa wanadhibiti maeneo ya Kusini, Magharibi, Kati, na Darfur Mashariki.

Baada ya kushambulia watu wa Darfur kwa mwaka mmoja na nusu, RSF sasa imechukuwa udhibiti wa mji wa el-Fasher, na kufanya Darfur nzima kuwa chini ya udhibiti wao.

Wakati huohuo kinachoendelea El-Fasher ni mauaji ya kimbari. Kuna sheria za vita lakini wapiganaji wa RSF hawazizingatii zote.

Picha za satelaiti zinaonesha makaburi ya halaiki na mauaji kila mahali. Ili kukomesha ukatili zaidi na kulinda haki za binadamu kunatakiwa kupawe kipaumbele duniani.

Kwa hiyo, dalili zote zinaonesha kuwa RSF itaendelea kukiuka sheria za haki za binadamu za kimataifa na utaratibu kwa binadamu.

Taarifa zinaonesha kuwa, kwa mfano, kiongozi wa wapiganaji anayejulikana kama “Abu Lulu” yeye mwenyewe amewaua na kuagiza kuuawa kwa raia wengi. Haya ni moja ya matukio mengi. Suala kuu hapa ni kuwa hakuna vikwazo vya uhakika.

Mwandishi, Tunç Demirtaş ni mhadhiri katika idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Mersin, Uturuki

Kanusho: Maoni ya mwandishi hayaakisi maoni, mitazamo na sera za uhariri za TRT Afrika.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar
Baraza la Maaskofu Tanzania lataka uwajibikaji kwa waliohusika na mauaji ya waandamanaji
Baraza la usalama la UN laongezea mwaka mmoja ujumbe wa amani wa Abyei
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano