| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Kamanda wa jeshi la Sudan atoa wito wa kuhamasisha umma dhidi ya RSF
Kamanda mwandamizi wa jeshi la Sudan ametoa wito kwa raia kuitikia ombi la kiongozi wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan wa kutaka waungane nchini nzima dhidi ya wapiganaji wa RSF.
Kamanda wa jeshi la Sudan atoa wito wa kuhamasisha umma dhidi ya RSF
Watu wasiopungua 40,000 wameuawa Sudan tangu vita vilipoanza Aprili 2023. / Picha: AP
tokea masaa 2

Kamanda mwandamizi wa jeshi la Sudan amewataka raia kuitikia wito wa Mkuu wa Majeshi Abdel Fattah al-Burhan kuungana na wenzao nchi nzima dhidi ya wapiganaji wa RSF.
Ali Hassan Bello, kamanda wa eneo la Kiulinzi la Blue Nile, aliwapongeza wanajeshi, vikosi washirika, na umma “kwa ushindi waliopata enep la Kordofan dhidi ya wapiganaji.”
“Ushidni tutaupata katika miji iliyobaki,” alisema katika taarifa iliyosomwa na shirika la habari la serikali SUNA.


Aliwaomba vijana wa Sudan kuitikia wito wa Mkuu wa Majeshi wa kutaka wajitolee dhidi ya wapiganji hao.

Wito wa nchi nzima
Siku ya Jumamosi, Burhan, ambaye ni mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Sudan, alitoa wito kwa nchi nzima dhidi ya wapiganaji wa RSF.
Siku ya Jumanne, jeshi lilisema kuwa limepata mafanikio makubwa katika maeneo kadhaa Kordofan baada ya makabiliano na RSF.
Jeshi limesema “maeneo muhimu” yako salama, na kuapa kuendelea na mapigano dhidi ya RSF “hadi nchi itakapokuwa haina uasi na ajenda ya mataifa ya kigeni.”
Wakati huohuo, Jeshi la Sudan limedungua ndege isiyokuwa na rubani siku ya Jumatano katika eneo la Al Obeid, mji mkuu wa Jimbo la Kordofan Kaskazini, walioshuhudia walisema.

Ushindi mkubwa kwa jeshi
Wanaharakati wa Sudan wameweka video katika mitandao ya kijamii zikionesha mitambo yao ya ulinzi yakidungua ndege zisizo na rubani kabla kuanguka.
Hakukuwa na taarifa yoyote kutoka kwa RSF kuhusu tukio hilo.

Siku ya Jumanne, muungano wa vikosi vinavyounga mkono jeshi, ulisema wamechukuwa udhibiti wa Abu Sunun na Abu Qaoud jimbo la Kordofan Kaskazini.
Siku moja kabla ya hapo, jeshi la Sudan lilisema limechukuwa tena eneo la Um Sayala huko Kordofan Kaskazini kutoka kwa RSF.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara
Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema
Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo
Wanajeshi wa RSF wameripotiwa kupata hasara kubwa katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan
CAF yatangaza wasimamizi maarufu wa sherehe ya Tuzo za CAF 2025
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar