| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa kwa jenerali wa jeshi
Brigedia huyo wa jeshi ndiye afisa wa ngazi ya juu kuuawa katika vita hivyo vya muda mrefu tangu 2021.
Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa kwa jenerali wa jeshi
Rais wa Nigeria Bola Tinubu ameomboleza kifo cha kamanda wa jeshi. MAKTABA
tokea masaa 21

Rais wa Nigeria Bola Tinubu amethibitisha siku ya Jumanne kuwa magaidi walimuua brigedia jenerali wa jeshi, afisa wa ngazi ya juu kufariki katika vita hivyo vya muda mrefu tangu 2021.

ISWAP ilidai siku ya Jumatatu kuwa ilimvamia na kumuua kamanda mmoja eneo la Chad kaskazini, wakionyesha picha ya Brigedia Jenerali Musa Uba.

"Nimeskitishwa na kifo hiki cha wanajeshi na maafisa wetu waliokuwa kwenye mapambano. Mungu awafariji familia za Brigedia Jenerali Musa Uba na mashujaa wengine," Tinubu alisema katika taarifa.

Kwanza jeshi la Nigeria lilipinga taarifa hizo kuwa Uba alikamatwa waliposhambuliwa.

Kulingana na taarifa ya jeshi na Umoja wa Mataifa, wanajeshi wawili na sungusungu wawili waliuawa katika shambulio hilo.

ISWAP ilijitenga na kundi la kigaidi la Boko Haram 2016 na limejielekeza katika kushambulia jeshi la Nigerian.

Mashambulizi ya kigaidi yamewaua watu zaidi ya 40,000 na kufanya watu karibu milioni mbili kaskazini mashariki mwa kuondolewa katika makazi yao tangu 2009, na yameendelea hadi katika nchi jirani ya Niger, Chad na Cameroon.

Uba ni afisa wa pili mwandamizi wa jeshi kuuawa na magaidi katika kipindi cha miaka minne, baada ya Jenerali Dzarma Zirkusu, aliyeuawa Novemba 2021.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara
Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema
Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo
Wanajeshi wa RSF wameripotiwa kupata hasara kubwa katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan
CAF yatangaza wasimamizi maarufu wa sherehe ya Tuzo za CAF 2025
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar