| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Rais Samia awatengua Nape na Makamba kutoka baraza lake la mawaziri
Rais amefanya mabadiliko kadhaa ikiwemo kuwateua mawaziri wapya, manaibu mawaziri na wengine katika nyadhifa mbali mbali.
Rais Samia awatengua Nape na Makamba kutoka baraza lake la mawaziri
Samia Suluhu Tanzania ametangaza  uteuzi wa Mawaziri mapya,  Manaibu Waziri na Makatibu wa mikoa./ Picha : Ikulu Tanzania 
22 Julai 2024

Rais wa Jamhuri ya Tanzania Samia Suluhu Hassan amemfuta kazi Nape Nnauye kama waziri wa habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, na badala yake kumtangaza Jerry William Slaa kuchukua wadhifa huo.

Kabla ya uteuzi huo, Slaa alikuwa akihudumu kama waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi.

Nape ambaye ndiye mbunge wa jimbo la Mtama mkoani Lindi, ameshika wadhifa huo wa waziri wa habari tangu mwaka 2022.

Ni mzoefu wa Diplomasia na Mahusiano ya Kigeni na Sayansi ya Jamii ambapo anashikilia shahada kutoka Kituo cha Mahusiano ya Nje na Chuo cha Sayansi ya Jamii cha Kivukoni, mtawalia. Kwa sasa, ni mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania.

Rais pia amempandisha cheo Ridhiwani Jakaya Kikwete kuwa waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, VIjana, Ajira na wenye ulemavu). Kabla ya uteuzi huu, Kikwete alikuwa naibu waziri, ofisi ya Rais, Menejimenti ya utumishi wa umma na Utawala bora

January Makamba pia ameondolewa kama waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, ambaye nafasi yake sasa itakchukuliwa na aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Italia Mahmoud Thabit Kombo.

Rais Samia hakutangaza Makamba atahamishwa kitengo kipi japo kumekuwa na mjadala mtandaoni wa uwezekano kuteuliwa kuwania Uenyekiti wa tume ya Umoja wa Afrika AU.

Iwapo kweli Makamba atawania Uenyekiti huo, basi atakuwa anjiunga katika kinyang'anyiro hicho na wagombea wengine kutoka Kenya na Djibouti.

Hii pia itaonekana kama kinyume na tangazo la hapo awali mwezi Machi, ambapo Rais wa Kenya William Ruto alitangaza kuwa Afrika Mashariki imekubaliana kumuunga mkono Mgombea mmoja kwa nafasi hiyo.

Rais Ruto alikuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa awali wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) katika mji mkuu wa Kenya Nairobi.

“Kwa mtazamo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, tumeshauriana kama wakuu wa nchi kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki, na tumekubali kudhamini mgombea mmoja kama wana Afrika Mashariki,'' Rais Ruto alisema.

Deogratius John Ndejembi amehamishwa kuwa waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Tangazo hilo la Rais pia lilijumuisha uteuzi wa Manaibu Waziri na Makatibu wa mikoa.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Bassirou Diomaye Faye: Rais wa Senegal
Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara
Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema
Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo
Wanajeshi wa RSF wameripotiwa kupata hasara kubwa katika jimbo la Kordofan Kaskazini nchini Sudan
CAF yatangaza wasimamizi maarufu wa sherehe ya Tuzo za CAF 2025
Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na  rubela
Rais wa Sudan Kusini Kiir amrejesha makamu wa rais katika mabadiliko ya baraza la mawaziri
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mlipuko wa virusi vya Marburg umethibitishwa kusini mwa Ethiopia
DR Congo, M23 wasaini makubaliano ya amani 'ya kihistoria' nchini Qatar