| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Afrika yamuomboleza waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga
Raila Odinga alikuwa akipata matibabu nchini India
Afrika yamuomboleza waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga
Raial odinga amefariki akiwa india kwa matibabu
15 Oktoba 2025

Salamu za rambirambi zinatoka sehemu tofauti ya bara la Afrika baada ya kifo cha aliyekuwa waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga. Odinga ameaga dunia nchini India Jumatano, ambapo alikuwa anapata matibabu.

“Tumempoteza kiongozi mahiri, mwanamajumui wa Afrika, mpenda amani na mtafuta suluhu, ambaye ushawishi na upendo wake haukuwa tu ndani ya Kenya, bali Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Msiba huu si wa Kenya pekee, bali wetu sote.” ameandika Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika ukurasa wake wa X.

“Kwa niaba ya Serikali na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninatuma salamu za pole kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Dkt. William Samoei Ruto, Mama Ida Odinga, watoto, familia, ndugu, jamaa, marafiki na wananchi wote wa Kenya kwa msiba huu,” aliongeza kusema Rais Samia katika ujumbe wake mtandaoni.

Nae Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ametoa ujumbe wake.

“Kwa niaba ya Serikali ya Ethiopia, natuma salamu zangu za rambirambi kwa kuondokewa na aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga. Apumzike Kwa amani,” Ahmed alisema katika akaunti ya X.

Nao uongozi wa Umoja wa Afrika pia umetoa salamu za rambirambi kufuatia kifo hicho.

"Raila Odinga alikuwa mtu mashuhuri katika maisha ya kisiasa ya Kenya na mpiganaji thabiti wa demokrasia, utawala bora na maendeleo yanayozingatia watu. Ahadi yake ya miongo kadhaa ya haki, wingi wa watu na mageuzi ya kidemokrasia iliacha alama isiyofutika sio tu kwa Kenya bali katika bara zima la Afrika,” mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Mahamoud Ali Youssouf alisema.

“Alihamasisha vizazi vya viongozi, pamoja na imani yake, ujasiri na ustahimilivu wa raia. mazungumzo na taasisi za kidemokrasia,” alisema Mwenyekiti.

Aliyekuwa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Moussa Faki naye ameandika rambirambi zake katika mtandawo wa kijamii.

“Ni kiongozi asiye na woga, Raila Odinga alitengeneza mkondo wa kisiasa wa nchi yake,” Faki alisema.

“Raila Odinga alitengeneza mkondo wa kisiasa wa nchi yake. Mtetezi mkubwa wa ushirikiano wa bara, pia aliitumikia kama Mwakilishi Mkuu wa Maendeleo ya Miundombinu. Rambirambi zangu nyingi kwa familia yake,” aliongezea.

Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’