| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Samia: Najivunia kumuenzi Magufuli kwa vitendo
Baada ya mkutano huo wa kampeni, Rais Samia alizuru kaburi la Magufuli ambako aliwasha mshumaa, alishiriki sala fupi ya kumuombea na kuweka shada la maua.
Samia: Najivunia kumuenzi Magufuli kwa vitendo
Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Samia Suluhu Hassan./Picha:@ccm_tanzania
14 Oktoba 2025

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Samia Suluhu Hassan amesema anajivunia kutekeleza dhamira ya mtangulizi wake, John Pombe Magufuli ya kuleta mabadiliko ndani ya nchi.

Akizungumza Oktoba 13, 2025 wakati wa mkutano wake wa kampeni uliofanyika mkoani Geita, Samia amesema kuwa miradi mingi mikubwa ya maendeleo aliyoianzisha Magufuli ameikamilisha.

"Nyote mtakubaliana na mimi nimetekeleza dhamira yake na shauku yake ya kuleta mabadiliko ndani ya nchi yetu," alisema Samia.

Kulingana na Samia, mtangulizi wake alimuachia ujenzi wa Bwawa la Kufua Umeme wa Maji la Julius Nyerere (JNHPP) ukiwa katika asilimia 37 na sasa amelikamilisha na kuzalisha umeme.

Alianisha mradi mwingine kuwa ni wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Dar es

Salaam hadi Morogoro ambao walianza pamoja, kabla ya kumuachia ukiwa asilimia 30, na sasa ameukamilisha na watu wanasafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma na vipande kadhaa vinaendelea kujengwa hadi Kigoma.

Mgombea huyo wa CCM alisisitiza kuwa aliliacha daraja la Kigongo Busisi lilkiwa asilimia 21, lakini kwa sasa watu wanapita kwa saa chache kwenda upande mmoja kwa miguu na vyombo vya moto.

Samia amelitaja suala la Serikali kuhamia Dodoma kama mradi mwingine ambao ulianzishwa na Magufuli na sasa Serikali, Bunge na Mahakama vyote viko Dodoma, na Mji wa Serikali wa Mtumba unaendelea kukamilishwa.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi