| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
DRC na waasi wa M23 wasaini makubaliano ya kutekeleza usitishaji mapigano
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na makundi ya waasi, yakiwemo waasi wa M23, wamesaini makubaliano mjini Doha ya kuanzisha utaratibu wa kufuatilia utekelezaji wa usitishaji mapigano, serikali ya Kongo imetangaza Jumanne.
DRC na waasi wa M23 wasaini makubaliano ya kutekeleza usitishaji mapigano
Waasi wa M23 walielezea mpango huo wa Jumanne kama hatua kubwa. /
14 Oktoba 2025

DRC na makundi ya waasi, yakiwemo AFC/M23, walisaini makubaliano hayo Jumanne mjini Doha ili kuweka mfumo wa ufuatiliaji wa usitishaji mapigano, ikiwa ni juhudi za hivi karibuni kumaliza machafuko mashariki mwa DRC.

Hafla ya utiaji saini ilifanyika chini ya uangalizi wa nchi ya Qatar, ambayo ndiyo nchi mpatanishi, na ilishuhudiwa na wawakilishi waangalizi kutoka Marekani, Umoja wa Afrika, na ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DRC (MONUSCO).

"Wajumbe kutoka DR Congo na River Alliance/M23 walisaini Jumanne mfumo wa ufuatiliaji na uthibitishaji wa usitishaji mapigano, chini ya uangalizi wa Qatar," Wizara ya Mawasiliano ya DRC ilisema kupitia ujumbe kwenye mtandao wa kijamii X.

Pande hizo zilitia saini makubaliano ya kanuni za kusitisha mapigano huko Doha mwezi Julai.

Hatua kubwa

Hata hivyo mapigano yanaendelea kati ya vikosi vya serikali na waasi wa M23, huku kila upande ukishutumu mwingine kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.

Serikali ilisema makubaliano ya Jumanne ni hatua kubwa katika utekelezaji wa kanuni za tamko zilizotiwa saini mnamo Julai 19.

Kwa kusainiwa makubaliano hayo, DRC "inathibitisha nia yake ya kufikia usitishaji wa vita, kudhamini usalama wa watu, na kuandaa mazingira ya makubaliano ya amani ya kudumu, ndani ya mfumo wa mchakato wa Doha unaoungwa mkono na jumuiya ya kimataifa," wizara hiyo ilisema.

M23 inaelezea mpango huo kama 'hatua kubwa'

Kundi hilo linadhibiti eneo kubwa, ikiwa ni pamoja na miji mikuu ya majimbo ya Goma na Bukavu, baada ya kuyateka mapema mwaka huu.

Umoja wa Mataifa, Kinshasa na wengine wanaishutumu nchi jirani ya Rwanda kwa kuunga mkono M23, jambo ambalo Kigali inakanusha.

Waasi wa M23 walielezea mpango huo wa Jumanne kama hatua kubwa.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’