AFRIKA
1 dk kusoma
Afrika Kusini yafuzu Kombe la Dunia 2026 baada ya kuifunga Rwanda
Afrika Kusini imekuwa taifa la hivi karibuni kutoka Afrika kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 baada ya kuichapa Rwanda mabao 3-0 siku ya Jumanne na kuongoza kundi C.
Afrika Kusini yafuzu Kombe la Dunia 2026 baada ya kuifunga Rwanda
Afrika Kusini imefuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 2010, ilipoandaa mashindano ya mwaka huo. / / Reuters
tokea masaa 9

Timu hiyo ya Bafana bafana imefuzu Kombe la Dunia licha ya kuondolewa pointi tatu kwa kumchezesha mchezaji asiyestahili katika mechi za awali.

Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Afrika Kusini kushiriki Kombe la Dunia tangu ilipofuzu moja kwa moja kama mwenyeji mwaka 2010.

Ushindi huo wa Afrika Kusini umeifanya Nigeria kumaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo, na sasa italazimika kushiriki hatua ya mchujo ili kufuzu.

Nigeria iliifunga Benin 4-0 nyumbani, baada ya mshambuliaji Victor Osimhen kufunga mabao matatu.

CHANZO:Reuters