| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Rais wa Madagascar avunja bunge huku mzozo wa kisiasa ukitikisa nchi
Agizo lililowekwa kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook lilisema Rais Andry Rajoelina alishauriana na viongozi wa bunge na Seneti kuhusu uamuzi huo.
Rais wa Madagascar avunja bunge huku mzozo wa kisiasa ukitikisa nchi
Waandamanaji wakiandamana katika mji wa Antananarivo, Madagascar, Oktoba 13. /
14 Oktoba 2025

Rais wa Madagascar Andry Rajoelina siku ya Jumanne alivunja bunge, na hiyvo kupindua azma ya bunge kumuondoa madarakani, iliyoongozwa na upinzani, kutokana na mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini humo.

Rajoelina amekabiliwa na zaidi ya wiki mbili za maandamano barabarani, yakiongozwa kwa kiasi kikubwa na waandamanaji vijana, na kumlazimisha kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 51 kujificha.

Agizo la kuvunja bunge "litaanza kutekelezwa mara moja baada ya kutangazwa kwenye redio na/au matangazo ya televisheni", ilisema taarifa ya rais katika ujumbe uliyowekwa kwenye Facebook.

Rajoelina, ambaye amekaidi wito unaoongezeka wa kumtaka ajiuzulu, alitetea hatua hiyo katika ujumbe tofauti kwenye mtandao wa kijamii kama muhimu "kurejesha utulivu ndani ya taifa letu na kuimarisha demokrasia."

"Lazima watu wasikike tena. Vijana wapewe nafasi," alisema kupitia mtandao wa kijamii.

Kumuondoa rais madarakani

Kiongozi wa upinzani Siteny Randrianasoloniaiko alisema Jumatatu watapiga kura kumshtaki Rajoelina kwa kukimbia kazini kufuatia ripoti kuwa aliikimbia nchi.

Rajoelina, meya wa zamani wa mji mkuu Antananarivo, alisema Jumatatu jioni alikuwa yuko "mahali salama" baada ya majaribio ya kumuua, bila kufichua eneo lake.

Maandamano hayo yalianza Septemba 25 na kufikia hatua muhimu mwishoni mwa juma wakati wanajeshi walioasi na vikosi vya usalama viliungana na waandamanaji hao na kumtaka rais na mawaziri wengine wa serikali kujiuzulu.

Miongoni mwao kulikuwa na kitengo cha CAPSAT, ambacho kilikuwa na jukumu kubwa katika mapinduzi ya 2009 ambayo kwanza yalimuweka Rajoelina madarakani.

Ili kujaribu kutuliza maandamano, rais mwezi uliopita alivunja serikali yake yote. Aliripotiwa kuhamishwa hadi Ufaransa kwa ndege ya kijeshi siku ya Jumapili baada ya makubaliano na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.

CHANZO:AFP
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’