tokea masaa 16
Tangu Septemba 27, waandamanaji wamekuwepo barabarani katika miji kadhaa nchini Morocco, wakipinga matumizi ya mabilioni ya fedha yanayoelekezwa katika maandalizi ya Kombe la Dunia 2030.
Vijana hao wanaojiita wanaharakati wa “Gen Z 212” wamekuwa wakiandamana katika maeneo ya viwanja vipya wakidai kutelekezwa kwa huduma za msingi za umma. Vijana hao wamehamasishana kupitia mitandao ya kijamii kama TikTok na mingineyo.
Hotuba hii inakuja wiki moja baada ya maandamano ya vijana ambao walituma barua moja kwa moja katika kasri la mfalme wakieleza malalamiko yao.
Walitaka kufutwa kazi kwa Waziri Mkuu Aziz Akhannouch na serikali yake, kuachiliwa huru kwa wafungwa wa kisiasa, na kuundwa kwa jukwaa litakalo wawajibisha wanasiasa mafisadi.
CHANZO:TRT Afrika Swahili