ULIMWENGU
1 dk kusoma
Marekani yapongeza azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu usalama wa Haiti
Uamuzi huo unakuja baada ya baraza hilo kuidhinisha kikosi kipya cha kulinda usalama nchini Haiti.
Marekani yapongeza azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu usalama wa Haiti
Wajumbe wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa./Picha:@UN_News_Centre
1 Oktoba 2025

Marekani imepongeza azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuidhinisha kikosi kipya cha kulinda usalama nchini Haiti, kijulikanacho kama ‘Gang Suppression Force (GSF)’.

Kikosi hicho, ambacho kitahudumu kwa miezi 12, kinachukua nafasi ya ‘Multinational Security Support (MSS)’, ambacho pia kilihusisha askari kutoka Kenya.

“Marekani itaendelea kufanya kazi na wadau mbalimbali kuisaidia Haiti iweze kupata amani na utulivu,” alisema Marco Rubio, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani.

Aliongeza: Ujumbe kutoka baraza hilo ni wazi kabisa: Wale wenye nia ya kuendeleza vurugu nchini Haiti, siku zao zimekwisha.

Azimio hilo, ambalo limefadhiliwa kwa pamoja na Panama na Marekani, pia limeidhinisha kuanzishwa kwa ofisi maalumu ya Uratibu ya Umoja wa Mataifa (UNSOH).

Wakati huo huo, Rubio aliopongeza Kenya na mataifa mengine yaliyochangia kwenye operesheni maalumu ya ulinzi wa amani Haiti, ambayo ilianza Juni 2024, ikifikia tamati Oktoba 2.

Zaidi ya watu milioni 1.3 wamekimbia makazi yao nchini Haiti kutokana na vurugu, idadi kubwa zaidi katika historia ya nchi hiyo na karibu nusu ya nchi inakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula.

 

CHANZO:AA
Soma zaidi
Maseneta wa Marekani wanamtaka Trump kuchukua msimamo thabiti dhidi ya unyakuzi wa West Bank
Waziri Mkuu wa Israel amfuta kazi msaidizi wake mkuu wa usalama kwa mtafaruku juu ya Gaza
Mbu wapatikana nchini Iceland kwa mara ya kwanza
Kiongozi Mkuu wa Iran, Khamenei, apinga madai kuwa Marekani imeharibu uwezo wa nyuklia wa nchi yake
Mashambulizi mapya ya Israel yawauwa takriban Wapalestina 21 huko Gaza licha ya kusitishwa kwa vita
Gaza inaishutumu Israel kwa wizi wa viungo kutoka kwa Wapalestina, inataka uchunguzi wa kimataifa
ICC inakataa ombi la Israel la kukata rufaa kuhusu vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na Gallant
Israel yapunguza upatikanaji wa misaada kwa nusu, inazuia mafuta kuingia Gaza
Mabomu ambayo hayajalipuka yana hatari 'kubwa' huko Gaza, NGO yaonya
Marekani katika kizungumkuti cha kutumia dhahabu yake kulipia deni la taifa
'Sura mpya kwa amani' — Dunia inajibu baada ya kusaini hati rasmi ya kumaliza vita vya Gaza
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Kuachiliwa kwa mateka kutaanza Gaza saa 11 alfajiri, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti
Israel inadhulumu wafungwa Wapalestina kabla ya kuachiliwa chini ya makubaliano na Hamas, video inaonyesha
Trump, Sisi kushirikiana kuandaa mkutano wa Gaza huko Sharm el-Sheikh nchini Misri
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2025
Wapalestina 200,000 wanarejea kaskazini mwa Gaza huku wanajeshi wa Israel wakiondoka
Wanajeshi wa Marekani wawasili Israel kusaidia kufuatilia usitishaji mapigano Gaza
Trump ataungana na viongozi, wanadiplomasia kutoka Uturuki na wengine kwenye mkutano wa Gaza, Cairo
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Nobel ya Amani 2025