ULIMWENGU
1 dk kusoma
Trump: Itakuwa ni ‘dhihaka’ kwa Marekani kama nisiposhinda Tuzo ya Amani ya Nobel
Siku ya Jumanne, Trump alisisitiza kuwa ameshiriki katika utatuzi wa migogoro saba, tangu kuingia kwake madarakani mwezi Januari mwaka 2025.
Trump: Itakuwa ni ‘dhihaka’ kwa Marekani kama nisiposhinda Tuzo ya Amani ya Nobel
Rais Donald Trump wa Marekani./Picha:Wengine
30 Septemba 2025

Rais wa Marekani Donald Trump amejinasibu kuwa anaweza kushinda Tuzo ya Amani ya Nobel, akiongeza kuwa itakuwa ni dhihaka kwa taifa lake iwapo ataikosa tuzo hiyo.

Akizungumza siku ya Jumanne, Trump amedai kuwa anastahili tuzo hiyo kutokana na nafasi yake katika usuluhishi wa migogoro na vita ulimwenguni.

Katika hotuba yake aliyoitoa siku ya Jumanne, Trump alisema kuwa alihusika na kusuluhisha migogoro saba ya kisiasa, tangu alipoingia madarakani mwezi Januari mwaka huu.

“Itakuwa dhihaka kubwa sana kwa nchi yetu, wacha nikuambie tu. Siihitaji tuzo hiyo binafsi, nataka nchi yangu ishinde,” alisema.

Trump, ambaye anatokea chama cha Republican, ameonekana kukerwa na uhalisia kwamba Barack Obama, kutoka Democrat aliwahi kushinda tuzo hiyo mwaka 2009.

Siku ya Jumanne, Trump alisisitiza kuwa ameshiriki katika utatuzi wa migogoro saba, tangu kuingia kwake madarakani mwezi Januari mwaka 2025.

Hivi karibuni, utawala wa Trump, ulianisha migogoro saba ambayo kiongozi huyo alihusika kuitatua ambayo ni Cambodia dhidi ya Thailand; Kosovo dhidi ya Serbia, DRC dhidi ya Rwanda, Pakistan dhidi ya India, Israel dhidi ya Iran, Misri dhidi ya Ethiopia na Armenia dhidi ya Azerbaijan.

CHANZO:AFP
Soma zaidi
Maseneta wa Marekani wanamtaka Trump kuchukua msimamo thabiti dhidi ya unyakuzi wa West Bank
Waziri Mkuu wa Israel amfuta kazi msaidizi wake mkuu wa usalama kwa mtafaruku juu ya Gaza
Mbu wapatikana nchini Iceland kwa mara ya kwanza
Kiongozi Mkuu wa Iran, Khamenei, apinga madai kuwa Marekani imeharibu uwezo wa nyuklia wa nchi yake
Mashambulizi mapya ya Israel yawauwa takriban Wapalestina 21 huko Gaza licha ya kusitishwa kwa vita
Gaza inaishutumu Israel kwa wizi wa viungo kutoka kwa Wapalestina, inataka uchunguzi wa kimataifa
ICC inakataa ombi la Israel la kukata rufaa kuhusu vibali vya kukamatwa kwa Netanyahu na Gallant
Israel yapunguza upatikanaji wa misaada kwa nusu, inazuia mafuta kuingia Gaza
Mabomu ambayo hayajalipuka yana hatari 'kubwa' huko Gaza, NGO yaonya
Marekani katika kizungumkuti cha kutumia dhahabu yake kulipia deni la taifa
'Sura mpya kwa amani' — Dunia inajibu baada ya kusaini hati rasmi ya kumaliza vita vya Gaza
Viongozi wa Marekani, Uturuki, Misri, na Qatar wamesaini makubaliano yanayositisha vita vya Gaza
Kuachiliwa kwa mateka kutaanza Gaza saa 11 alfajiri, vyombo vya habari vya Israel vinaripoti
Israel inadhulumu wafungwa Wapalestina kabla ya kuachiliwa chini ya makubaliano na Hamas, video inaonyesha
Trump, Sisi kushirikiana kuandaa mkutano wa Gaza huko Sharm el-Sheikh nchini Misri
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2025
Wapalestina 200,000 wanarejea kaskazini mwa Gaza huku wanajeshi wa Israel wakiondoka
Wanajeshi wa Marekani wawasili Israel kusaidia kufuatilia usitishaji mapigano Gaza
Trump ataungana na viongozi, wanadiplomasia kutoka Uturuki na wengine kwenye mkutano wa Gaza, Cairo
Kiongozi wa upinzani wa Venezuela Maria Corina Machado ashinda Tuzo ya Nobel ya Amani 2025