AFRIKA
1 dk kusoma
Sudan yatoa wito kwa dunia kushtumu 'uhalifu' wa RSF dhidi ya raia
Mapigano kati ya jeshi la Sudan, na wapiganaji wa RSF yameongezeka kote Kordofan, na maeneo ya Darfur katika wiki za hivi karibuni.
Sudan yatoa wito kwa dunia kushtumu 'uhalifu' wa RSF dhidi ya raia
Msudan ambaye alilazimika kuondoka katika makazi yake aungana tena na familia yake baada ya kukimbia mji wa Al Fasher, Septemba 6, 2025. / Reuters
tokea masaa 14

Sudan imetaka jamii ya kimataifa na mashirika ya kikanda ya haki za binadamu kushtumu “uhalifu” unaofanywa na wapiganaji wa RSF dhidi ya raia na kuchukuwa hatua za haraka kuzuia hayo.

“Serikali ya Sudan inashtumu vikali uhalifu na ukiukwaji unaoendelea ambao unafanywa na wapiganaji wa RSF dhidi ya raia wasio na hatia, wasio na silaha, na kuharibu taasisi za serikali kwa maksudi, ikiwa ni ukiukwaji wa wazi wa haki za binadamu na maadili ya kimataifa,” Baraza la Kijeshi lilisema katika taarifa siku ya Jumamosi.

Lilisema serikali ‘‘inatoa wito kwa jamii ya kimataifa na mashirika ya haki za binadamu ya kikanda kushtumu ukatili unaoendelea na kuchukua hatua za haraka kuzuia uhalifu wa wapiganaji hao na kuwawajibisha wahusika, ili kulinda raia na kusimamia haki za binadamu”.

Mapema siku ya Jumamosi, jeshi la Sudan lilitangaza kuwa limefanya mashambulizi makubwa dhidi ya RSF huko Al Fasher, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa Sudan, kutoka maeneo matano, katika moja ya mapigano makali kuwahi kutokea kwenye mji huo katuka miezi kadhaa.

Katika wiki za hivi karibuni, mapigano kati ya jeshi la Sudan na wapiganaji wa RSF yameongezeka kote katik majimbo ya Kordofan na Darfur.

CHANZO:AA