| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Watu wasiopungua 13 wauawa, 19 wajeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya RSF huko Darfur Sudan
Raia wasiopungua 13 wameuawa na wengine 19 kujeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya wapiganaji wa RSF Kaskazini mwa Darfur, madaktari wa eneo hilo wamesema siku ya Jumatatu.
Watu wasiopungua 13 wauawa, 19 wajeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya RSF huko Darfur Sudan
Watu wasiopungua 20,000 wameuawa kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe Sudan tangu vilipoanza katikati ya mwezi April 2023./ Picha: AP
6 Oktoba 2025

Raia wasiopungua 13 wameuawa na wengine 19 kujeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya wapiganaji wa RSF Kaskazini mwa Darfur, madaktari wa eneo hilo wamesema siku ya Jumatatu.

Mtandao wa Madaktari wa Sudan unasema watu waliojeruhiwa wanajumuisha watoto saba na mwanamke mmoja mjamzito katika shambulio lililolenga eneo la makazi huko El-Fasher, mji kuu wa Kaskazini mwa Darfur magharibi mwa Sudan.

Kundi hilo la madaktari linasema raia kadhaa walikuwa bado wamekwama huku eneo hilo likishambuliwa.

lilishtumu mashambulizi hayo ya RSF kama “uhalifu kamili na kulenga kwa maksudi maisha ya raia,huku jamii ya kimataifa ikiwa imenyamaza kimya bila kuona aibu na kushindwa kulinda maisha ya maelfu ya wakazi waliokwama kwenye mji huo.”

Wito wa hatua za haraka

Kundi hilo limetoa wito kwa jamii ya kimataifa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuchukuwa hatua za haraka kuzuia mashambulizi dhidi ya raia na kuhakikisha raia wanalindwa pamoja na wafanyakazi wa afya.

RSF imeweka vizuizi El-Fasher tangu Mei 10, 2024, licha ya onyo la kimataifa kuhusu hatari kwa mji huo, ambapo shughuli za kutoa misaada kwa majimbo yote matano ya Darfur zimekuwa zikifanyika.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’