AFRIKA
1 dk kusoma
Urusi na Ethiopia zasaini mpango wa kuanzisha mradi wa nishati ya nyuklia
Urusi na Ethiopia zimesaini mpango wa kuanzisha mradi wa ujenzi wa kiwanda cha nishati ya nyuklia katika nchi hiyo ya Afrika, shirika la habari la TASS limeripoti.
Urusi na Ethiopia zasaini mpango wa kuanzisha mradi wa nishati ya nyuklia
Rais wa Urusi Vladimir Putin alikuwa mwenyeji wa Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed mnamo Septemba 25, 2025. / / AP
tokea masaa 13

Urusi na Ethiopia, zilisaini mpango wa kuanzisha mradi wa kiwanda cha nishati siku ya Alhamisi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Rosatom, Alexey Likhachev, na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia, Gedion Timotheos, walisaini mkataba huo jijini Moscow mbele ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin, na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed.

Pande zote mbili pia zilisisitiza ushirikiano katika sekta za nishati na miundombinu.

Rosatom ni shirika la serikali la Urusi linalohusika na nishati ya atomiki, lililoanzishwa mwaka 2007.

Nchi hizo mbili zilisaini makubaliano kuhusu ushirikiano katika matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia mwaka 2017, ambayo yaliweka msingi wa ushirikiano mpana zaidi katika sayansi ya nyuklia, teknolojia na elimu.