| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa ADF wameua watu 19 mashariki mwa DRC
Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa ADF wamewauwa watu 19 katika shambulio la usiku moja mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na kuzidisha ukosefu wa usalama katika eneo hilo lenye utajiri wa madini
Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa ADF wameua watu 19 mashariki mwa DRC
Watu wanaoshukiwa kuwa waasi wa ADF wamewaua takriban watu 19 katika shambulio jipya mashariki mwa DRC. / Picha: Reuters
14 Oktoba 2025

Washukiwa wa waasi wa ADF wamewaua raia 19 katika shambulio la usiku huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), maafisa wawili wa eneo hilo walisema Jumatatu, hali inayozidi kuzorotesha usalama katika eneo hilo lenye utajiri wa madini.

Shambulio hilo, linalodhaniwa kufanywa na kundi la Allied Democratic Forces (ADF), lilitokea katika kijiji cha Mukondo kilichopo mkoa wa Kivu Kaskazini, alisema Alain Kiwewa, msimamizi wa kijeshi wa eneo la Lubero ambako Mukondo iko, akiongeza kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka.

Hakukuwa na madai ya haraka ya uwajibikaji kutoka kwa ADF, ambayo imewahi kudai kuhusika na mashambulio kadhaa katika miezi ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na shambulio moja mnamo Septemba kwenye mazishi ambalo liliua zaidi ya raia 60.

Washambuliaji huko Mukondo walivaa sare zinazofanana na zile za jeshi la Kongo, jambo lililowaruhusu kuingia kijijini bila kushukiwa. Kisha waliwashambulia watu kwa kutumia bunduki, visu, na marungu, alisema mchungaji wa eneo hilo ambaye alikataa kutaja jina lake kwa sababu za kiusalama.

Nyumba zilichomwa moto

Kiongozi mmoja wa jamii ya kiraia kutoka eneo hilo, Espoir Kambale, pia alisema idadi ya waliouawa ni 19 na kuongeza kuwa watu wengine wanane walijeruhiwa na nyumba 26 zilichomwa moto.

"Tunajiuliza jinsi waasi walivyoweza kuja na kutushambulia wakati tuliamini kijiji kimeimarishwa kiusalama," alisema Kambale. "Wananchi wako katika hali ya hofu. Baadhi ya wakazi walikimbilia msituni na hawajarudi."

ADF ilianza kama kundi la waasi nchini Uganda lakini limekuwa likifanya makazi katika misitu ya nchi jirani ya DRC tangu mwishoni mwa miaka ya 1990.

Mashambulio yake ya hivi karibuni yameongeza hofu ya kiusalama mashariki mwa DRC, ambako waasi wa M23 walifanya mashambulizi makubwa mwaka huu, hali iliyosababisha utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump kujaribu kupatanisha amani.

CHANZO:Reuters
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’