AFRIKA
1 dk kusoma
Tanzania: Yanga yatwaa taji la Ngao ya Jamii ikiifunga Simba 1-0
Bao pekee la ‘Wananchi’ lilipatikana katika dakika 53 ya mchezo, kupitia kwa mchezaji wao nyota, Pacome Zouzoua, na hivyo kuifanya Simba kupoteza mchezo wao wa sita mfululizo katika michezo tofauti, mbele ya mahasimu wao wa jadi.
Tanzania: Yanga yatwaa taji la Ngao ya Jamii ikiifunga Simba 1-0
Wachezaji wa Young Africans wakishangilia ubingwa wao mara baada ya kuifunga Simba kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii./Picha:@YoungAfricansSC
16 Septemba 2025

Simba Sports Club imeendeleza ‘uteja’ wake mbele ya mahasimu wao Young Africans, baada ya kufungwa bao 1-0, katika mchezo wa Ngao ya Jamii, uliofanyika Septemba 16, 2025, katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la ‘Wananchi’ lilipatikana katika dakika 53 ya mchezo, kupitia kwa mchezaji wao nyota, Pacome  Zouzoua, na hivyo kuifanya Simba kupoteza mchezo wao wa sita mfululizo katika michezo tofauti, mbele ya mahasimu wao wa jadi.

CHANZO:TRT Afrika Swahili