| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Umoja wa Afrika yamchagua Rais wa Uganda kuwa mpatanishi wa amani Sudan
Vita nchini Sudan vimekuwepo tangu Aprili 2023 na kusababisha maelfu kuhama makazi yao na wengine kukimbilia nchi za nje.
Umoja wa Afrika yamchagua Rais wa Uganda kuwa mpatanishi wa amani Sudan
Rais Yoweri Museveni ameteuliwa kuongoza mchakato wa amani nchini Sudan/ picha: Reuters / Reuters
31 Oktoba 2025

Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, limemuelekeza Mwenyekiti wa Tume ya AU ashirikiane kwa haraka na Wajumbe wa Kamati ya Madhubuti ya Rais ya PSC, chini ya uongozi wa Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Uganda, ili kuwezesha haraka mchakato wa mazungumzo kati ya viongozi wa Jeshi la Sudan (SAF) na wapiganaji wa kundi la Rapid Support Forces (RSF) ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa Mkutano Maalum wa AU kuhusu Sudan.

“Kwa vitendo vya uhalifu dhidi ya raia wa Sudan na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na sheria za kimataifa, unaofanywa na RSF, baraza linatoa wito kwa kiongozi wa jeshi la RSF kuzingatia sheria ya kimataifa kwa haki za kibinadamu.” imesema katika taarifa.

Vita nchini Sudan vimekuwepo tangu Aprili 2023 na kusababisha maelfu kuhama makazi yao na wengine kukimbilia nchi za nje.

Baraza limetoa “ madai ya kusitishwa mara moja na bila masharti ya uhasama na kufunguliwa kwa njia salama ili kuruhusu misaada ya kuokoa maisha kuwafikia watu walioathirika huko El Fasher na kuonya kuwa wahusika wa vitendo hivyo vya kikatili watawajibishwa.”

“Baraza linaomba Tume ya AU kufuatilia mara kwa mara na kuripoti uhalifu huo wa kutisha unaofanywa kote nchini Sudan, ili kuweka hatua za kuzuia na kupunguza hatari ya kutokea tena; kuendeleza mapendekezo ya jinsi ya kushughulikia ili kuzuia kuongezeka kwao zaidi; kuunda mpango wa ulinzi wa raia, na kutoa mapendekezo kwa PSC ndani ya wiki tatu;

CHANZO:TRT Swahili
Soma zaidi
Afrika Kusini yaomba utulivu kufuatia maandamano dhidi ya kusimikwa kwa 'Igwe' wa Nigeria
Rwanda ‘yahofia’ operesheni za DRC dhidi ya kikundi cha FDLR
Kenya yalipa ada ya Dola milioni 30 ya uenyeji wa AFCON 2027
Hasara ya mamilioni kufuatia ubomoaji katika soko kubwa zaidi la wazi la Gikomba Nairobi
Shabiki maarufu ‘Lumumba Vea’ akosa viza ya  kwenda kuishangilia DRC dhidi ya Jamaica
Mamlaka ya uchukuzi Kenya yazindua ukaguzi wa lazima wa afya kwa madereva ili kupunguza ajali
Tanzania yahimiza matumizi ya AI kuimarisha mtangamano na maendeleo EAC
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 Jimbo la Plateau nchini Nigeria
Wafungwa wasiopungua 11 wafariki kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jela DRC
Kagame awaamuru maafisa waandamizi wa serikali 'kusimama' wakati wa hotuba yake
Wadukuzi wadukua maombi ya kazi 450,000 nchini Afrika Kusini
Rais wa Misri asema ni Trump pekee anaweza kusimamisha vita, aonya kupanda zaidi kwa bei ya mafuta
Togo yatoa uzoefu wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele
Watu 15 wamefariki katika ajali ya barabarani mkoa wa kati Kenya
Mahakama kuu ya Jamhuri ya Congo imethibitisha ushindi wa Sassou Nguesso kwa awamu ya tano
Rwanda, Burundi wanagombana juu ya juhudi za rais wa zamani wa Senegal Sall kuongoza UN
Vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya vyaongezeka hadi 108, polisi wasema
Majenerali wakuu wa Uganda wazuiliwa kwa madai ya ufisadi: ripoti
Eswatini yamrudisha nyumbani mwananchi wa Cambodia aliyefukuzwa kutoka Marekani
Waasi waanza kuondoka katika vijiji vya DRC ili kuhimiza amani