AFRIKA
1 dk kusoma
Wafanyakazi watano wa kujitolea wauawa Sudan wakiwa wanasambaza chakula, kulingana na IFRC
Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu (IFRC) limesema Jumanne kuwa wafanyakazi wake watano wa kujitolea wameuawa Sudan.
Wafanyakazi watano wa kujitolea wauawa Sudan wakiwa wanasambaza chakula, kulingana na IFRC
Shirika la IFRC limesema wafanyakazi wengine watatu hawajulikani walipo. / / Reuters
tokea masaa 5

Wafanyakazi hao watano wameuawa katika jiji la Bara wakiwa wanagawanya chakula na wakiwa wamevaa vazi rasmi la shirika hilo, lisema IFRC, bila kutoa maelezo ya jinsi walivyouwawa au kumtaja yeyote aliyehusika.

Shirika hilo pia limesema wafanyakazi wengine watatu hawajulikani walipo.

Jeshi la Sudan na kikosi cha wanamgambo cha Rapid Support Forces (RSF) wamekuwa wakipigana tangu Aprili 2023, mapigano ambayo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 20,000 na kuwafurusha watu milioni 14, kulingana na Umoja wa Mataifa na mamlaka za ndani.

CHANZO:Reuters