| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Julius Malema apatikana na hatia ya kufyatua risasi kwenye mkutano
Julius Malema alishtakiwa kukiuka Sheria ya kumiliki na kudhibiti silaha na huenda akafungwa jela hadi miaka 15.
Julius Malema apatikana na hatia ya kufyatua risasi kwenye mkutano
Chama cha Malema kilipata asilimia 10 ya kura katika uchaguzi mkuu uliopita. / Getty
1 Oktoba 2025

Kiongozi wa upinzani wa Afrika Kusini Julius Malema alipatikana na hatia siku ya Jumatano ya kukiuka sheria ya kumiliki silaha katika tukio la mwaka 2018 ambapo alionekana kwenye video akifyatua risasi katika mkutano wa kisiasa.

Mwanasiasa huyo jasiri, ambaye anaongoza chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters, alishtakiwa kwa kukiuka Sheria ya Kudhibiti Silaha.

Malema huenda akafungwa gerezani hadi miaka 15, lakini kwa kuwa hakuna kifungo cha chini kabisa, hakimu anaweza kumhurumia. Hukumu kuhusu kifungo chake itatolewa Januari 23 mwakani.

Mlinzi wake binafsi wakati huo Adriaan Snyman, ambaye anadaiwa kumpa Malema bunduki hiyo, pia alishtakiwa lakini hakupatikana na hatia. Malema anasema alithibitisha kuwa hakimu alikuwa ni mbaguzi wa rangi, kwa sababu Snyman ni jina la kizungu.

Sherehe za maadhimisho ya chama

Video hiyo ya Malema akifyatua risasi wakati wa maadhimisho ya miaka mitano ya chama chake mkoa wa Eastern Cape ilisambazwa sana 2018. Kundi la wahamasishaji wa Kiafrikaner, Afriforum, liliwasilisha kesi hiyo ya uhalifu dhidi yake.

Katika kujitetea, Malema alidai kuwa bunduki iliyoonekana kwenye video ilikuwa ni ya watoto kuchezea, lakini hili lilikataliwa na hakimu Twanet Olivier.

Malema amewaambia wanaomuunga mkono nje ya Mahakama ya East London kuwa atakata rufaa ya hukumu hiyo hadi katika Mahakama ya Katiba.

Alianzisha chama cha Economic Freedom Fighters, chama cha nne kwa ukubwa nchini Afrika Kusini, ambacho kilipata ushindi wa asilimia 9 katika uchaguzi mkuu wa mwaka uliopita.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’