| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mgomo wa wafanyakazi wa mafuta Nigeria wasitishwa
Wizara ya Kazi imeeleza kwamba wafanyakazi walioachishwa kazi watapewa kazi katika sehemu nyingine za Kundi la Dangote bila kupoteza mshahara.
Mgomo wa wafanyakazi wa mafuta Nigeria wasitishwa
Picha ya Maktaba: Wizara ya Kazi imesema kwamba walioachishwa kazi watapewa ajira sehemu nyengine.
1 Oktoba 2025

Muungano wa wafanyakazi wa mafuta nchini Nigeria umekubali kusitisha mgomo baada ya mkutano na uongozi wa Dangote Petroleum pamoja na maafisa wa serikali, Wizara ya Kazi ya nchi hiyo imesema.

Mgomo huo ulianzishwa baada ya kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote - ambacho ni kikubwa zaidi barani Afrika na kina uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 ya mafuta kwa siku - kuwasimamisha zaidi ya wafanyakazi 800 waliokuwa wamejiunga na muungano.

Hatua hiyo ya mgomo ilikuwa imeweka hatarini usambazaji wa mafuta na biashara katika eneo la Afrika Magharibi.

Wizara ya Kazi ilisema katika taarifa baada ya mkutano wa upatanishi kati ya muungano wa PENGASSAN na Dangote Petroleum kwamba wafanyakazi waliokuwa wamefukuzwa watapewa nafasi za kazi katika sehemu nyingine za kundi la Dangote bila kupoteza mishahara yao.

Waziri wa Kazi alisisitiza katika mkutano huo kwamba kujiunga na muungano ni haki ya wafanyakazi na inapaswa kuheshimiwa.

"PENGASSAN wamekubali kuanza mchakato wa kusitisha mgomo," taarifa hiyo iliongeza.

“Wafanyakazi katika kiwanda cha kusafisha mafuta cha Dangote, ambacho kinamilikiwa binafsi, walifukuzwa kazi siku ya Alhamisi kwa sababu ya kujiunga na muungano, PENGASSAN,” ilisema siku ya Ijumaa.

Maafisa wa kiwanda cha Dangote walisema wakati huo kwamba kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao kulikuwa sehemu ya mpango wa kupanga upya wafanyakazi na waliwatuhumu walioathirika kwa vitendo vya hujuma.

Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’