| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
ZEC: Wapiga kura 8,325 Zanzibar wakosa sifa
Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imeidhinisha jumla ya wapiga kura 717,557 watakaoshiriki kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.
ZEC: Wapiga kura 8,325 Zanzibar wakosa sifa
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa ZEC, Thabit Idarous Faina./Picha:Wengine
1 Oktoba 2025

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imetangaza kuwa jumla ya wapiga kura 717,557 ndiyo waliodhinishwa kushiriki katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, mara baada ya kukamilika kwa mchakato wa uhakika wa daftari la kudumu la wapiga kura.

Kulingana na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa ZEC, Thabit Idarous Faina, jumla ya wapiga kura 8,325 wameondolewa katika daftari hilo kutokana na kukosa sifa.

Kati ya wapigakura waliodhinishwa, wanawake ni 378,334, ambayo ni sawa na asilimia 53, huku wanaume wakiwa 339, 223, sawa na asilimia 47.

Kati ya idadi hiyo, vijana wenye umri wa miaka 18 hadi 35 ni 326,304(asilimia 45), wenye umri wa miaka 36 hadi 59 ni 300,986(asilimia 42) na walio na umri wa miaka 59 na kuendelea ni 90,267 ambayo ni sawa na asilimia 13.

“Hii ndiyo nguvu ya kisiasa iliyo mbele yenu, Ni wajibu wenu wanasiasa kufahamu namna ya kuwafikia wapigakura hawa ili kuwashawishi katika kampeni,”alisema Faina, wakati wa mkutano na wadau wa uchaguzi visiwani humo.

Wakati uchaguzi wa Tanzania bara ukisimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC), uchaguzi wa Zanzibar unasimamiwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Tanzania Bara ina jumla ya wapiga kura milioni 36,929,683. Hii ni ongezeko la wapiga kura milioni 7.9 sawa na asilimia 26.6 toka wapiga kura milioni 29,754,696 waliosajiliwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

 

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi