| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Samia: Wananchi tukapige kura usalama ni mkubwa
Kulingana na Samia, wale wanaoshawishi kuvunja amani wana mahali pa kukimbilia wao na familia zao.
Samia: Wananchi tukapige kura usalama ni mkubwa
Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Samia Suluhu Hassan./Picha:@ccm_tanzania
1 Oktoba 2025

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan amewataka wanachama wote wa chama hicho na Watanzania kwa ujumla wajitokeze kwa wingi Oktoba 29 na kwenda kupiga kura, na wasikubali kushawishika kuvunja amani ya nchi.

Samia ameyasema hayo Oktoba 1, 2025, wakati wa kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu, katika mji wa Bomang'ombe wilayani Hai Mkoa wa Kilimanjaro, akiwa njiani kuelekea Arusha.

Mgombea huyo, amewahimiza wana CCM na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kupiga kura na kuinyanyua CCM ili wanaoitazama Tanzania kwa jicho lingine 'waweke heshima'.

"Tukipiga kura kwa wingi, tukiinyanyua CCM kwa wingi, wale wanaoitazama Tanzania kwa jicho lingine wataweka heshima sawasawa," alisema Samia.

Ameongeza: "La pili ninalotaka kuwaambia ndugu zangu msikubali kushawishiwa, mkikubali kushawishiwa tutaharibu amani ya nchi yetu ya Tanzania. Msikubali hata kidogo".

Kulingana na Samia, wale wanaoshawishi kuvunja amani wana mahali pa kukimbilia wao na familia zao.

"Wanaoshawishi wanapo pa kwenda nataka kuwaambia likitokea jambo kidogo tunawakuta Airport (kiwanja cha ndege) pasipoti zao mkononi zina viza tayari wanaondoka, familia zao haziko hapa. Wanachochea kufanya fujo kukikorogeka wakimbie wakaungane na familia zao, sisi tunakwenda wapi? Kwetu ni hapahapa Tanzania, tuilinde nchi yetu kwa wivu mkubwa."

Amewasisitiza vijana wasikubali hilo na wakapige kura na kurejea nyumbani kusubiri matokeo.

"Kwa hiyo nawaomba vijana wangu, watoto wangu, vijana Watanzania msikubali hata kidogo, tokeni kapigeni kura rudi nyumbani subiri matokeo.

Ninawahakikishia usalama na vyombo vya ulinzi vimejipanga vema kutakuwa salama, lakini na ninyi wananchi mtunze usalama," aliongeza.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’