| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mkuu wa haki za binadamu UN atoa wito wa kuzuiwa 'ukatili mkubwa zaidi' El Fasher, Sudan
Raia wamezuiwa kutoka Darfur Kaskazini, njaa, mashambulizi yanayoongezeka, anaonya Volker Turk
Mkuu wa haki za binadamu UN atoa wito wa kuzuiwa 'ukatili mkubwa zaidi' El Fasher, Sudan
Volker Turk
2 Oktoba 2025

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya haki za binadamu ametoa wito wa kuchukuliwa hatua kwa lengo la kuzuia "ukatili mkubwa zaidi, kwa misingi ya kikabila na maafa" huko El Fasher, mji mkuu wa eneo la Kaskazini la Sudan la Darfur, ambapo wapiganaji wa RSF wamezuia watu kutoka kwa zaidi ya siku 500.

"El Fasher iko kwenye hali ya janga kubwa iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa kuwalinda raia," Volker Turk alisema katika taarifa.

Raia wasiopungua 91 waliuawa kati ya Septemba 19-29 kwenye mashambulizi ya makombora ya RSF, ndege zisizokuwa na rubani, na mashambulizi ya ardhini, kulingana na ofisi ya masuala ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa.

Kumekuwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika nyumba, masoko, miskiti, na maeneo ya kupika chakula cha jamii yanayolenga kulazimisha watu kuhama makazi yao, ikiwemo kutoka kwa kambi ya Abu Shouk ambayo watu walioondoka makazi yao wanaishi kwa sasa.

Turk ameonya kuhusu msururu wa ukatili kwa misingi ya kikabila, ikiwemo udhalilishaji wa kingono unaolenga wanawake na wasichana wa jamii ya Zaghawa, kama ilivyoshuhudiwa mwanzoni mwa mashambulizi ya RSF. Alitoa wito wa kuwepo kwa njia salama, na kuruhusu raia wanaotaka kuondoka kwa hiari waondoke, kama vile wazee na wagonjwa, na kutaka kusiwe na vizuizi kwa ajili ya misaada kwa watu.

"Hakuna bidhaa muhimu na bei zinapanda zaidi, raia wako katika hatari ya njaa," amesema, akishtumu vikwazo vya RSF na taarifa za mateso na mauaji kwa kuingiza chakula kimagendo.

"Ukatili uko wazi," mkuu huyo wa masuala ya haki za binadamu alisisitiza na kuongeza: "Haya yanaweza kuepukwa kama wadau wote watachukuwa hatua madhubuti za kuhakikisha sheria ya kimataifa inatekelezwa na maisha ya raia yanalindwa."

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi