| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Ahueni kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri bei za mafuta zikishuka mwezi Oktoba
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji nchini Tanzania (EWURA), imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli zitakazotumika kuanzia Oktoba 1, 2025.
Ahueni kwa wamiliki wa vyombo vya usafiri bei za mafuta zikishuka mwezi Oktoba
Bei ya mafuta yazidi kushuka nchini Tanzania./Picha:Wengine
1 Oktoba 2025

Bei za mafuta ya petroli na dizeli zitakazotumika Oktoba mwaka huu nchini Tanzania, zimeendelea kupungua kwa kiwango tofauti ikilinganishwa na zilizokuwepo mwezi uliotangulia, huku upande wa mafuta ya taa ukiendelea kusalia vilevile.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Tanzania (EWURA), punguzo la gharama za nishati hizo, zinakuwa wakati kukiwa na ongezeko katika soko la dunia kwa asilimia 2.80 kwa mafuta ya petroli, asilimia 3.65 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 3.57 kwa mafuta ya taa.

Kwa jiji la Dar es Salaam, lita moja ya petrol itakuwa inapatikana kwa Dola 1.11 (Shilingi 2,720) kutoka Dola 1.14 (2,807) kama ilivyokuwa kwa mwezi wa Septemba.

Taarifa hiyo, ambayo imesainiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa EWURA, James Mwainyekule imeongeza kuwa gharama za kubadilisha fedha za kigeni zimepungua kwa asilimia 5.10.

“Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta katika vituo vinavyouza mafuta kwa bei nafuu zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja,” ilisomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Mamlaka hiyo imesisitiza kuwa bei za bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko, kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015, kifungu namba 166.

Pia, imevitaka vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana yakionesha bei za mafuta, punguzo, vivutio vya kibiashara vinavyotolewa na kituo husika.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi