Afisa Mkuu Mtendaji wa kampuni ya Exxon Darren Woods alieleza wasiwasi wake kuhusu hatari ya kundi la waasi katika eneo la kaskazini mashariki la Cabo Delgado, ambapo Exxon inapanga kujenga kiwanda kikubwa zaidi cha gesi barani Afrika, ripoti ilisema, ikinukuu vyanzo vinavyofahamu mazungumzo hayo.
Wapiganaji wanaohusishwa na kundi la Islamic State walianzisha uasi katika mkoa wa Cabo Delgado wenye utajiri mkubwa wa gesi mwaka 2017, na kuwaua maelfu ya raia, kutatiza maisha ya watu na kulazimisha maelfu wengine kuhama makazi yao, kulingana na mashirika ya misaada. Uasi huo umetatiza miradi ya nishati yenye thamani ya mabilioni ya madola.
Woods na Chapo pia walijadilli mipango ya TotalEnergies kuanzisha tena mradi wao wa gesi katika kiwanda cha karibu.
TotalEnergies ilikuwa imesitisha mradi huo 2021 baada ya wapiganaji kuvamia mji wa kaskazini wa Palma, kituo muhimu karibu na panapochimbwa gesi.